Dkt.Mwigulu aiagiza wizara ya Nishati kuongeza kasi usambazaji gesi asilia

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App


Na Mwandishi wetu,Dar

 
WAZIRI MKUU, Dkt. Mwigulu Nchemba ameiagiza Wizara ya Nishati kuongeza kasi ya kupanua mtandao wa usambazaji wa gesi asilia ili kukidhi mahitaji ya Taifa.

Amesema kwa kufanya hivyo kutawawezesha wananchi kupata nafuu ya gharama katika uendeshaji wa vyombo vya moto na matumizi mengine ya nishati pamoja na Serikali kupunguza matumizi ya fedha za kigeni kuagiza mafuta.

Amesema hayo leo Februari 09, 2026 alipozindua kituo Mama cha Gesi Asilia Iliyosindikwa (CNG) cha Puma Energies kilichopo Salasala jijini Dar es Salaam. Ujenzi wa kituo hicho umegarimu takriban shilingi bilioni 13.

“Wizara ya Nishati pia endeleeni kuongeza kasi ya utafutaji wa gesi asilia ili iwe nishati ya kawaida ya maisha ya kila siku ya Mtanzania, Watanzania wote jitokezeni kwa wingi kutumia fursa ya uwepo wa gesi asilia iliyoshindiliwa”.

Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa uzinduzi wa mradi huo unaakisi utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Nishati na Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050. “Vilevile, inaendana na mwelekeo wa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan wa  kuhakikisha rasilimali za nishati, hususan gesi asilia zinatumika kama kichocheo cha maendeleo ya viwanda, usafiri na uzalishaji wa umeme”.

Amesema mradi huo unaashiria hatua muhimu katika utekelezaji wa mkakati wa Taifa wa kuhamia kwenye matumizi ya nishati safi, salama, nafuu na ya uhakika kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii. "Kwa kufanya haya Puma Energies mmeunga mkono kwa vitendo jitihada za Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za kuijenga Tanzania inayotumia nishati safi.”

Kadhalika Mheshimiwa Dkt. Mwigulu amesema kuwa Serikali itaendelea kuchukua hatua za kuboresha mazingira ya uwekezaji ikiwemo kuhakikisha uwepo wa sera thabiti, mifumo rafiki ya udhibiti, uwazi katika utoaji wa maamuzi na ushirikiano wa karibu kati ya taasisi za Serikali na sekta binafsi.

“Serikali inathamini sana mchango wa Sekta Binafsi katika kutekeleza Miradi ya Maendeleo na utoaji wa huduma kwa umma, Serikali imeendelea kushirikiana na sekta binafsi katika ujenzi wa vituo vya gesi asilia iliyoshindiliwa”.

Waziri Mkuu amesema kuwa katika kipindi cha siku 100 za Rais Dkt. Samia madarakani, Serikali imewezesha upatikanaji wa majiko banifu 13,575 yenye ruzuku ya asilimia 85 na Mitungi ya LPG 28,653 ya kilo sita (6) yenye ruzuku ya asilimia 50. “Vilevile, Serikali imewezesha Taasisi 89 zinazolisha watu zaidi ya 100 kwa siku kuhamia katika matumizi ya nishati safi ya kupikia na hivyo kufikia jumla ya taasisi 1,136.”

Naye Naibu Waziri Wizara ya Nishati, Salome Makamba amesema kuwa moja ya maeneo yanayokua kwa kasi katika matumizi ya gesi asilia ni sekta ya usafirishaji kupitia matumizi ya Gesi Asilia Iliyoshindiliwa (CNG), ambapo kwa sasa zaidi ya vyombo vya moto 15,000 nchini vinatumia CNG.

Amesema kuwa hadi kufikia Januari 2026, vituo vya kujazia CNG vilikuwa 11 ambapo 9 viko katika Jiji la Dar es Salaam, kimoja kipo Mkoa wa Pwani na kingine kipo Mtwara.

“Serikali kwa kushirikiana na sekta binafsi tumeweka mpango wa kuongeza idadi ya vituo kufikia 20 ifikapo Juni, 2026 hususani katikamikoa ya Morogoro na Dodoma, ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma za CNG katika miji mikubwa na kwenye barabara kuu za usafirishaji”
Share:

Makamu wa Rais azindua Moangi wa Ushirikiano kati ya Taasisi za elimu na viwanda

  1. Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App



Na Mwandishi wetu ,Dar

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi ametoa wito kwa sekta binafsi kushirikiana na Vyuo, kuwekeza katika tafiti hususan za sayansi na teknolojia ili kuinua viwango vya tafiti na ubora wa elimu nchini.
 
Makamu wa Rais amesema hayo wakati wa uzinduzi wa mpango wa ushirikiano kati ya Taasisi za Elimu na Waajiri, uliyofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es Salaam. Amesema Kupitia Mpango huo, sekta binafsi inaweza kuchangia maendeleo ya elimu kwa kufadhili tafiti na kutoa ufadhili kwa wanafunzi wa fani mbalimbali kulingana na mahitaji ya soko la ajira.
 
Aidha, Makamu wa Rais ametoa wito kwa Taasisi za elimu na Sekta binafsi nchini kuzingatia maendeleo ya kasi ya sayansi na teknolojia duniani katika utekelezaji wa Mpango huo. Amesema Vyuo na Sekta binafsi vishirikiane kubaini ujuzi muhimu unaohitajika sasa na siku zijazo hususan katika fani za sayansi, teknolojia, ubunifu, tiba, uhandisi na hesabu ili kuwezesha vijana kushindana na kupata nafasi katika soko la ajira  nchini na kimataifa.
 
Makamu wa Rais amesema ushirikiano baina ya Taasisi za elimu na Viwanda ni hitaji la lazima katika dunia ya leo, kwa kuwa Vyuo haviwezi tena kuwa visiwa vya nadharia, na viwanda haviwezi kukua bila nguvukazi yenye ujuzi unaoendana na teknolojia na ushindani wa soko.

Ameongeza kwamba, Serikali ya Awamu ya Sita imeweka kipaumbele cha kimkakati katika kukuza ujuzi, stadi, maarifa na sifa za kuajirika au kujiajiri miongoni mwa vijana na wahitimu wa ngazi mbalimbali za elimu, ikitambua kwamba maendeleo endelevu ya Taifa hayawezekani bila kuwa na rasilimaliwatu iliyoelimika na yenye uwezo wa kuchangia kikamilifu katika uchumi wa Taifa.

Amesema Serikali imeendelea kufanya maboresho makubwa ya sera na mitaala ya elimu katika ngazi zote kwa lengo la kuujenga mfumo wa elimu ulio mnyumbufu, jumuishi na unaoendana na vipaji, mwelekeo na mahitaji halisi ya soko la ajira, huku ikizingatia mabadiliko ya teknolojia na ushindani wa kitaifa na kimataifa.

Uzinduzi wa Mpango huo ni utekelezaji wa ahadi ya Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025, ambapo aliahidi kuanzisha Mpango wa pamoja kati ya Waajiri, Vyuo vya ufundi stadi na Vyuo Vikuu kwa lengo la kulinganisha mafunzo na mahitaji halisi ya sekta za kipaumbele za Taifa, ndani ya siku 100 baada ya kuapishwa kwake.

Pamoja na mambo mengine, Mpango wa ushirikiano kati ya Taasisi za Elimu na Viwanda unalenga kuimarisha uhusiano wa kimkakati kati ya utoaji wa elimu na utendaji kazi, kwa lengo la kulinganisha mafunzo na mahitaji ya sekta za kipaumbele kama nishati, Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA) na viwanda vya kuongeza thamani. 

Aidha, Mpango unaweka msingi thabiti wa kujenga kizazi cha wahitimu wenye uwezo wa kuajirika, kujiajiri na kushiriki kikamilifu katika maendeleo ya Taifa kwani umedhamiria kubadilisha mfumo wa elimu ya nadharia kwenda mfumo unaozingatia ujuzi, vitendo, ubunifu na uzalishaji mali.

Uzinduzi huo, umehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali, Bunge, Dini pamoja na wadau wa maendeleo. Wengine waliohudhuria ni pamoja na Waajiri na Wamiliki wa Viwanda, Wakuu wa Taasisi mbalimbali, Wakuu wa Vyuo pamoja na Wanafunzi.
 

Share:

MENEJIMENTI YA TMDA YAJIPANGA NA DIRA 2050

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App




Na Mwandishi wetu

Menejimenti ya TMDA yakutana Morogoro  Februari 3-4, 2026 kujadili rasimu ya Mpango Mkakati Mpya wa Mamlaka wa miaka mitano, 2026/27-2030/31 unaoakisi utekelezaji wa Dira ya Taifa ya 2050. 

Rasimu ya Mpango Mkakati huo ni ya Sita kufuatia kukamilika kwa ufanisi kwa Mpango Mkakati wa Tano. Mpango Mkakati wa Sita wa TMDA unatarajiwa kuanza kutumika mnamo tarehe 01, Julai, 2026.

Pamoja na mambo mengine, rasimu ya Mpango Mkakati husika inalenga katika kuhakikisha ubora, usalama na ufanisi wa bidhaa za dawa, vifaa tiba na vitendanishi kwa lengo la kulinda afya ya Jamii. 

Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, Dkt. Adam Fimbo, aliwaeleza wajumbe wa kikao husika kuwa rasimu husika ya Mpango Mkakati inabeba Dira mpya ya TMDA ambayo ni "Kuimarika kwa afya na ustawi wa Watanzania wote kupitia udhibiti bora unaokidhi viwango vya kitaifa". 

Dkt. Fimbo aliongeza kuwa,  Dhamira Mpya ya Taasisi itakuwa " Kulinda  Afya ya Jamii kwa kuhakikisha, usalama, ubora na ufanisi wa dawa, vifaa tiba, vitendanishi na bidhaa zote zinazohusiana na afya".

Uongozi wa TMDA imekuwa na utamaduni shirikishi katika kujadili mambo makubwa yahusuyo taasisi, ambapo watumishi wote hushirikishwa kupitia ngazi mbalimbali ndani ya Mamlaka kabla ya kuidhinishwa na Bodi ya Ushauri ya Wizara kwa TMDA (MAB).

Pamoja na mambo mengine, Mpango Mkakati huu mpya unaweka mwelekeo wa pamoja katika udhibiti, utasaidia katika kupanga matumizi ya rasilimali vizuri na kuboresha uwajibikaji na uwazi.

Mpango Mkakati wa TMDA ni nyaraka muhimu ambayo inaonesha ramani ya safari ya taasisi na ndiyo chombo muhimu cha kuongoza maamuzi na maendeleo ya TMDA.


Share:

Baraza la sita la wafanyakazi lachagiza mafanikio ya TMDA

Published from Blogger Prime Android App


Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App


Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App


Na Mwandishi wetu,Morogoro

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya  Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) , Dkt. Adam Fimbo, ametoa pongezi kwa wajumbe wa Baraza la Sita la Wafanyakazi wa TMD kufuatia muda wake wa kuhudumu kufikia kikomo. 

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kikao cha mwisho cha Baraza hilo la Wafanyakazi lililofanyika  5 Februari, 2026 mkoani Morogoro, Dkt. Fimbo amesema kuwa Baraza la Sita la wafanyakazi ambalo limedumu kwa miaka mitano  limekuwa na mchango mkubwa katika mafanikio ya TMDA katika kipindi hiki ambayo yametokana na mahusiano mazuri baina ya uongozi na wafanyakazi kupitia ushirikishwaji wa wafanyakazi kwenye maamuzi makubwa yenye kuleta tija kwa taasisi kupitia vikao mbalimbali vya baraza.

Dkt . Fimbo amesema, katika kipindi cha baraza hili, mafanikio makubwa ya yaliyopatikana ndani ya TMDA ni pamoja na;  kukamilika kwa jengo la ofisi ya TMDA Makao Makuu, Dodoma, kukamilika kwa nyumba za taasisi katika vituo vya mipaka vya Namanga na Tarakea na Ujenzi wa Tanuru la kuteketeza bidhaa duni na bandia kwa lengo la kulinda Afya ya Jamii. 

Aidha, Dkt. Fimbo ameongeza kuwa mafanikio mengine ambayo Baraza hili linalomaliza muda wake  limehusika nayo ni pamoja na TMDA kufikia ngazi ya 3 ya ukomavu ya WHO (WHO ML3) na kuiweka Tanzania kuwa nchi ya kwanza barani Afrika kufikia hadhi hiyo; Maabara kutambuliwa na WHO kuwa miongoni mwa Maabara bora duniani. Aidha, TMDA imeteuliwa na WHO kuwa Kituo cha Umahiri cha udhibiti wa  dawa, chanjo na utoaji mafunzo ya kiudhibiti barani Afrika.

Pia, Baraza hili la Sita limekuwa na mchango katika kuhakikisha TMDA inaweka mazingira mazuri ya uanzishaji na uendelezaji wa viwanda vya dawa za binadamu 19, dawa za mifugo 2 na vifaa tiba 41 nchini, amesema Dkt. Fimbo

Naye mwakilishi wa Ofisi ya TUGHE Makao Makuu, Wkl. Mwanaidi Mgowa amepongeza uongozi wa TMDA kwa kuwa na Baraza la Wafanyakazi la mfano wa kuigwa na Mabaraza mengine. Aidha, Wkl. Mgowa ametoa wito kwa wajumbe wa TUGHE kujitokeza kwa wingi kushiriki katika uchaguzi ngazi ya Mkoa na Taifa utakaofanyika ndani ya mwaka 2026.

Akitoa salamu za Kamishna wa kazi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano, Bw. Peter Sembuyagi ameupongeza uongozi wa TMDA kwa kufikia mafanikio makubwa ambayo yamepatikana kupitia dhana ya ushirikishaji ambalo ni takwa la kisheria mahala pa kazi.

Baraza la Wafanyakazi la TMDA hudumu kwa kipindi cha miaka mitano na linaundwa na Menejimenti, wajumbe wa TUGHE na wawakilishi kutoka katika ofisi zote za Kanda ambapo hukutana mara mbili kwa mwaka kwa lengo la kujadili masuala makubwa ya kitaasisi ikiwa ni njia moja wapo ya ushirikishaji wa watumishi katika ngazi ya maamuzi.
Share:

Waziri Makonda:Milango ipo wazi kwa UMIKIDO

Published from Blogger Prime Android App


DODOMA

Katika kuendelea kuimarisha umoja na kujitambulisha kwa Mamlaka mbalimbali, Mwenyekiti wa Umoja wa Vyombo vya Habari Mitandaoni Mkoa wa Dodoma (UMIKIDO), Benny Majata, amefanya mazungumzo mafupi na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda, katika Viwanja vya Bunge jijini Dodoma leo Januari 29, 2026

Katika mazungumzo hayo, sambamba na kujitambulisha kwa Waziri Makonda, Majata amemweleza kuhusu malengo ya kuanzishwa kwa UMIKIDO, ikiwemo kusimamia maudhui yenye weledi, kuhamasisha maadili ya habari mtandaoni, pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya vyombo vya habari na Serikali.

Kwa upande wake, Waziri Makonda amesema milango ya Wizara ipo wazi kwa UMIKIDO kufika ofisini kwa ajili ya kufanya mazungumzo ya kina juu ya namna Wizara itakavyoweza kusaidia umoja huo kutimiza malengo yake.











Share:

Miaka 64 ya Uhuru: TBN Yasema “Amani Kwanza, Ujenzi wa Taifa Daima”



Published from Blogger Prime Android App



Na Mwandishi wetu

Leo Desemba 9, tunapoadhimisha miaka 64 tangu Taifa la Tanzania  lipate Uhuru, Tanzania Bloggers Network (TBN) inawapongeza Watanzania wote kwa kufikia hatua hii muhimu katika historia ya Taifa letu. Hii ni siku ya kutafakari safari tuliyotoka, mahali tulipo, na mwelekeo tunaoujenga kwa pamoja.

Waasisi wetu walituwachia zawadi kubwa—Uhuru. Lakini walituonya kuwa Uhuru hauwezi kuwa kamili bila kujitegemea. Leo tunakumbusha maneno ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aliyewahi kusisitiza:

"Uhuru hauwezi kukamilika pasipo kujitegemea. Hatuwezi kuitwa huru kama tunategemea wengine kutupatia mahitaji yetu ya kimsingi."
 
Tujenge Taifa Letu – Tusiibomoe Tanzania

Kama mtandao wa habari za kidijitali, TBN inasisitiza kuwa mafanikio yetu kama Taifa yametokana na utulivu, umoja na mshikamano. Ili kuendelea mbele, tunahitaji kudumisha amani na maridhiano—nguzo muhimu za maendeleo.

Rais mstaafu Benjamin William Mkapa alituasa kwa busara:

"Amani si kitu cha asili; tunahitaji kuilinda na kuitunza kila siku. Bila amani, hakuna maendeleo ya kweli."

Tukikubali kuongozwa na chuki, uchochezi na vurugu, juhudi za waasisi wetu za kupambana na ujinga, umaskini na maradhi zitapotea. Tusiitumie mitandao au uhuru wa maoni kuharibu Taifa letu; tuitumie kulijenga.
Kila Zama na Kiongozi Wake – Tuunge Mkono Mageuzi

Kila kizazi kina wajibu wake. Kama alivyoeleza Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi:

"Kila utawala na zama zake. Kila kiongozi na mchango wake katika ujenzi wa Taifa hili."

Katika awamu ya sasa chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Tanzania inaendelea na mwelekeo wa 4R: Reconciliation, Resilience, Reforms, and Rebuilding. Huu ni mwaliko kwa Watanzania wote kushiriki katika kujenga Taifa lenye maridhiano, mageuzi chanya na uimara wa kiuchumi na kijamii.

Tuna nafasi ya kuzungumza—basi tuseme kwa njia inayojenga, si inayobomoa. Kuthamini Uhuru ni kufanya kazi kwa bidii, kulinda amani, na kuacha kutumiwa kuharibu misingi ya Taifa letu.
 
TBN Inawatakia Maadhimisho Mema ya Miaka 64 ya Uhuru!

Tanzania Kwanza — Kazi, Utu na Mshikamano. Tusonge Mbele!

Beda Msimbe
Mwenyekiti, Tanzania Bloggers Network (TBN)
Share:

Serikali Yaendelea Kuwezesha Vijana Kupata Fursa za Maendeleo – Maganga*


Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App


Published from Blogger Prime Android App



Na Mwandishi wetu,Mbeya

Serikali chini ya uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inaendelea kutekeleza mikakati kuhakikisha vijana wanapata fursa sawa za kujiletea maendeleo binafsi na kuchangia katika ustawi wa Taifa kwa ujumla.

Mikakati hiyo inajumuisha uanzishaji wa mifumo ya kitaasisi, kisera, mipango kazi, miongozo na sheria zinazolenga kutatua changamoto zinazowakabili vijana katika nyanja tofauti za kijamii na kiuchumi.

Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bi. Mary Maganga wakati wa Ufunguzi wa Kongamano la siku mbili la Vijana Tanzania linalofanyika kuanzia leo 12 Oktoba hadi 13 Oktoba, 2025 Jijini Mbeya katika Ukumbi wa City Park Garden.

Bi. Mary Maganga, amesema lengo la kongamano hilo ni kuwajengea vijana ujuzi na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika mabadiliko ya kijamii na kiuchumi, kukuza ushirikiano na ubadilishanaji wa mawazo, pamoja na kutambua na kuunga mkono mipango na miradi ya vijana inayolenga kuinua uchumi wao.

“Vijana ni nguvu ya mabadiliko na maendeleo katika jamii zetu. Ni lazima tutumie vema nguvu hii kubadilisha dunia kuwa mahali bora kwa ajili ya wote,” amesema Katibu Mkuu huyo.

Aidha, amewataka vijana kutumia kongamano hilo kama fursa ya kujifunza, kubadilishana uzoefu na kujadili changamoto zinazowakabili, ili Serikali iweze kuyachukua maoni yao na kuyatumia kuboresha sera, sheria, kanuni na miongozo kwa manufaa ya Vijana wote nchini.

Sambamba na hilo, Bi. Mary amewahimiza vijana kote nchini kujitokeza kushiriki katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025, kwa kuchagua viongozi wanaoakisi matumaini, malengo na ndoto za taifa hili.
Awali Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya Rodrick Mpogolo aliwasihi vijana kuendelea kuipenda nchi na kujivunia Taifa la Tanzania kwa kuwa ni mahala ambapo kila kijana ana mchango wa kuleta maendeleo.
Akizungumza kuhusu idadi ya washiriki wa kongaamano hilo Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu Seleman Mvunye alisema limehusisha zaidi ya vijana 1,500 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar pamoja na Maafisa Vijana toka Halmashauri zote nchini.

MWISHO.
Share:

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Labels

Recent Posts

Unordered List

  • Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  • Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  • Vestibulum auctor dapibus neque.

Pages

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.