Baraza la sita la wafanyakazi lachagiza mafanikio ya TMDA

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App


Published from Blogger Prime Android App


Na Mwandishi wetu,Morogoro

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya  Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) , Dkt. Adam Fimbo, ametoa pongezi kwa wajumbe wa Baraza la Sita la Wafanyakazi wa TMD kufuatia muda wake wa kuhudumu kufikia kikomo. 

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa Kikao cha mwisho cha Baraza hilo la Wafanyakazi lililofanyika  5 Februari, 2026 mkoani Morogoro, Dkt. Fimbo amesema kuwa Baraza la Sita la wafanyakazi ambalo limedumu kwa miaka mitano  limekuwa na mchango mkubwa katika mafanikio ya TMDA katika kipindi hiki ambayo yametokana na mahusiano mazuri baina ya uongozi na wafanyakazi kupitia ushirikishwaji wa wafanyakazi kwenye maamuzi makubwa yenye kuleta tija kwa taasisi kupitia vikao mbalimbali vya baraza.

Dkt . Fimbo amesema, katika kipindi cha baraza hili, mafanikio makubwa ya yaliyopatikana ndani ya TMDA ni pamoja na;  kukamilika kwa jengo la ofisi ya TMDA Makao Makuu, Dodoma, kukamilika kwa nyumba za taasisi katika vituo vya mipaka vya Namanga na Tarakea na Ujenzi wa Tanuru la kuteketeza bidhaa duni na bandia kwa lengo la kulinda Afya ya Jamii. 

Aidha, Dkt. Fimbo ameongeza kuwa mafanikio mengine ambayo Baraza hili linalomaliza muda wake  limehusika nayo ni pamoja na TMDA kufikia ngazi ya 3 ya ukomavu ya WHO (WHO ML3) na kuiweka Tanzania kuwa nchi ya kwanza barani Afrika kufikia hadhi hiyo; Maabara kutambuliwa na WHO kuwa miongoni mwa Maabara bora duniani. Aidha, TMDA imeteuliwa na WHO kuwa Kituo cha Umahiri cha udhibiti wa  dawa, chanjo na utoaji mafunzo ya kiudhibiti barani Afrika.

Pia, Baraza hili la Sita limekuwa na mchango katika kuhakikisha TMDA inaweka mazingira mazuri ya uanzishaji na uendelezaji wa viwanda vya dawa za binadamu 19, dawa za mifugo 2 na vifaa tiba 41 nchini, amesema Dkt. Fimbo

Naye mwakilishi wa Ofisi ya TUGHE Makao Makuu, Wkl. Mwanaidi Mgowa amepongeza uongozi wa TMDA kwa kuwa na Baraza la Wafanyakazi la mfano wa kuigwa na Mabaraza mengine. Aidha, Wkl. Mgowa ametoa wito kwa wajumbe wa TUGHE kujitokeza kwa wingi kushiriki katika uchaguzi ngazi ya Mkoa na Taifa utakaofanyika ndani ya mwaka 2026.

Akitoa salamu za Kamishna wa kazi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano, Bw. Peter Sembuyagi ameupongeza uongozi wa TMDA kwa kufikia mafanikio makubwa ambayo yamepatikana kupitia dhana ya ushirikishaji ambalo ni takwa la kisheria mahala pa kazi.

Baraza la Wafanyakazi la TMDA hudumu kwa kipindi cha miaka mitano na linaundwa na Menejimenti, wajumbe wa TUGHE na wawakilishi kutoka katika ofisi zote za Kanda ambapo hukutana mara mbili kwa mwaka kwa lengo la kujadili masuala makubwa ya kitaasisi ikiwa ni njia moja wapo ya ushirikishaji wa watumishi katika ngazi ya maamuzi.
Share:

Menejimenti ya TMDA yajipanga utekelezaji Dira 2050

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App


Na Mwandishi wetu

Menejimenti ya TMDA yakutana Morogoro  Februari 3 -4 2026 kujadili rasimu ya Mpango Mkakati Mpya wa Mamlaka wa miaka mitano, 2026/27-2030/31 unaoakisi utekelezaji wa Dira ya Taifa ya 2050. 

Rasimu ya Mpango Mkakati huo ni ya Sita kufuatia kukamilika kwa ufanisi kwa Mpango Mkakati wa Tano. Mpango Mkakati wa Sita wa TMDA unatarajiwa kuanza kutumika mnamo tarehe 01, Julai, 2026.

Pamoja na mambo mengine, rasimu ya Mpango Mkakati husika inalenga katika kuhakikisha ubora, usalama na ufanisi wa bidhaa za dawa, vifaa tiba na vitendanishi kwa lengo la kulinda afya ya Jamii. 

Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, Dkt. Adam Fimbo, aliwaeleza wajumbe wa kikao husika kuwa rasimu husika ya Mpango Mkakati inabeba Dira mpya ya TMDA ambayo ni "Kuimarika kwa afya na ustawi wa Watanzania wote kupitia udhibiti bora unaokidhi viwango vya kitaifa". 

Dkt. Fimbo aliongeza kuwa,  Dhamira Mpya ya Taasisi itakuwa " Kulinda  Afya ya Jamii kwa kuhakikisha, usalama, ubora na ufanisi wa dawa, vifaa tiba, vitendanishi na bidhaa zote zinazohusiana na afya".

Uongozi wa TMDA imekuwa na utamaduni shirikishi katika kujadili mambo makubwa yahusuyo taasisi, ambapo watumishi wote hushirikishwa kupitia ngazi mbalimbali ndani ya Mamlaka kabla ya kuidhinishwa na Bodi ya Ushauri ya Wizara kwa TMDA (MAB).

Pamoja na mambo mengine, Mpango Mkakati huu mpya unaweka mwelekeo wa pamoja katika udhibiti, utasaidia katika kupanga matumizi ya rasilimali vizuri na kuboresha uwajibikaji na uwazi.

Mpango Mkakati wa TMDA ni nyaraka muhimu ambayo inaonesha ramani ya safari ya taasisi na ndiyo chombo muhimu cha kuongoza maamuzi na maendeleo ya TMDA.


Share:

Waziri Makonda:Milango ipo wazi kwa UMIKIDO

Published from Blogger Prime Android App


DODOMA

Katika kuendelea kuimarisha umoja na kujitambulisha kwa Mamlaka mbalimbali, Mwenyekiti wa Umoja wa Vyombo vya Habari Mitandaoni Mkoa wa Dodoma (UMIKIDO), Benny Majata, amefanya mazungumzo mafupi na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Paul Makonda, katika Viwanja vya Bunge jijini Dodoma leo Januari 29, 2026

Katika mazungumzo hayo, sambamba na kujitambulisha kwa Waziri Makonda, Majata amemweleza kuhusu malengo ya kuanzishwa kwa UMIKIDO, ikiwemo kusimamia maudhui yenye weledi, kuhamasisha maadili ya habari mtandaoni, pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya vyombo vya habari na Serikali.

Kwa upande wake, Waziri Makonda amesema milango ya Wizara ipo wazi kwa UMIKIDO kufika ofisini kwa ajili ya kufanya mazungumzo ya kina juu ya namna Wizara itakavyoweza kusaidia umoja huo kutimiza malengo yake.











Share:

Miaka 64 ya Uhuru: TBN Yasema “Amani Kwanza, Ujenzi wa Taifa Daima”



Published from Blogger Prime Android App



Na Mwandishi wetu

Leo Desemba 9, tunapoadhimisha miaka 64 tangu Taifa la Tanzania  lipate Uhuru, Tanzania Bloggers Network (TBN) inawapongeza Watanzania wote kwa kufikia hatua hii muhimu katika historia ya Taifa letu. Hii ni siku ya kutafakari safari tuliyotoka, mahali tulipo, na mwelekeo tunaoujenga kwa pamoja.

Waasisi wetu walituwachia zawadi kubwa—Uhuru. Lakini walituonya kuwa Uhuru hauwezi kuwa kamili bila kujitegemea. Leo tunakumbusha maneno ya Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, aliyewahi kusisitiza:

"Uhuru hauwezi kukamilika pasipo kujitegemea. Hatuwezi kuitwa huru kama tunategemea wengine kutupatia mahitaji yetu ya kimsingi."
 
Tujenge Taifa Letu – Tusiibomoe Tanzania

Kama mtandao wa habari za kidijitali, TBN inasisitiza kuwa mafanikio yetu kama Taifa yametokana na utulivu, umoja na mshikamano. Ili kuendelea mbele, tunahitaji kudumisha amani na maridhiano—nguzo muhimu za maendeleo.

Rais mstaafu Benjamin William Mkapa alituasa kwa busara:

"Amani si kitu cha asili; tunahitaji kuilinda na kuitunza kila siku. Bila amani, hakuna maendeleo ya kweli."

Tukikubali kuongozwa na chuki, uchochezi na vurugu, juhudi za waasisi wetu za kupambana na ujinga, umaskini na maradhi zitapotea. Tusiitumie mitandao au uhuru wa maoni kuharibu Taifa letu; tuitumie kulijenga.
Kila Zama na Kiongozi Wake – Tuunge Mkono Mageuzi

Kila kizazi kina wajibu wake. Kama alivyoeleza Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi:

"Kila utawala na zama zake. Kila kiongozi na mchango wake katika ujenzi wa Taifa hili."

Katika awamu ya sasa chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Tanzania inaendelea na mwelekeo wa 4R: Reconciliation, Resilience, Reforms, and Rebuilding. Huu ni mwaliko kwa Watanzania wote kushiriki katika kujenga Taifa lenye maridhiano, mageuzi chanya na uimara wa kiuchumi na kijamii.

Tuna nafasi ya kuzungumza—basi tuseme kwa njia inayojenga, si inayobomoa. Kuthamini Uhuru ni kufanya kazi kwa bidii, kulinda amani, na kuacha kutumiwa kuharibu misingi ya Taifa letu.
 
TBN Inawatakia Maadhimisho Mema ya Miaka 64 ya Uhuru!

Tanzania Kwanza — Kazi, Utu na Mshikamano. Tusonge Mbele!

Beda Msimbe
Mwenyekiti, Tanzania Bloggers Network (TBN)
Share:

Serikali Yaendelea Kuwezesha Vijana Kupata Fursa za Maendeleo – Maganga*


Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App


Published from Blogger Prime Android App



Na Mwandishi wetu,Mbeya

Serikali chini ya uongozi wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inaendelea kutekeleza mikakati kuhakikisha vijana wanapata fursa sawa za kujiletea maendeleo binafsi na kuchangia katika ustawi wa Taifa kwa ujumla.

Mikakati hiyo inajumuisha uanzishaji wa mifumo ya kitaasisi, kisera, mipango kazi, miongozo na sheria zinazolenga kutatua changamoto zinazowakabili vijana katika nyanja tofauti za kijamii na kiuchumi.

Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bi. Mary Maganga wakati wa Ufunguzi wa Kongamano la siku mbili la Vijana Tanzania linalofanyika kuanzia leo 12 Oktoba hadi 13 Oktoba, 2025 Jijini Mbeya katika Ukumbi wa City Park Garden.

Bi. Mary Maganga, amesema lengo la kongamano hilo ni kuwajengea vijana ujuzi na uwezo wa kushiriki kikamilifu katika mabadiliko ya kijamii na kiuchumi, kukuza ushirikiano na ubadilishanaji wa mawazo, pamoja na kutambua na kuunga mkono mipango na miradi ya vijana inayolenga kuinua uchumi wao.

“Vijana ni nguvu ya mabadiliko na maendeleo katika jamii zetu. Ni lazima tutumie vema nguvu hii kubadilisha dunia kuwa mahali bora kwa ajili ya wote,” amesema Katibu Mkuu huyo.

Aidha, amewataka vijana kutumia kongamano hilo kama fursa ya kujifunza, kubadilishana uzoefu na kujadili changamoto zinazowakabili, ili Serikali iweze kuyachukua maoni yao na kuyatumia kuboresha sera, sheria, kanuni na miongozo kwa manufaa ya Vijana wote nchini.

Sambamba na hilo, Bi. Mary amewahimiza vijana kote nchini kujitokeza kushiriki katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025, kwa kuchagua viongozi wanaoakisi matumaini, malengo na ndoto za taifa hili.
Awali Katibu Tawala Mkoa wa Mbeya Rodrick Mpogolo aliwasihi vijana kuendelea kuipenda nchi na kujivunia Taifa la Tanzania kwa kuwa ni mahala ambapo kila kijana ana mchango wa kuleta maendeleo.
Akizungumza kuhusu idadi ya washiriki wa kongaamano hilo Mkurugenzi wa Maendeleo ya Vijana Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi,Vijana,Ajira na Wenye Ulemavu Seleman Mvunye alisema limehusisha zaidi ya vijana 1,500 kutoka Tanzania Bara na Zanzibar pamoja na Maafisa Vijana toka Halmashauri zote nchini.

MWISHO.
Share:

Brigaedia Jenerali Ndagala afungua kongamano la wadau wa Usimamizi wa Maafa Mbeya

Published from Blogger Prime Android App
Published from Blogger Prime Android App
Published from Blogger Prime Android App
Published from Blogger Prime Android App


 

Wadau watakiwa kutoa mapendekezo yenye tija kuboresha usimamizi wa maafa nchini


Na Mwsnfisho wetu,MBEYA

MKURUGENZI wa Idara ya Menejimenti ya Maafa, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Brigedia Jenerali Hosea Ndagala amefungua Kongamano la Wadau wa Usimamizi wa Maafa linalofanyika kama sehemu ya maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Kupunguza Athari za Maafa kwa mwaka 2025.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kongamano hilo leo 12 Oktoba 2025 jijini Mbeya, Brigedia Jenerali Ndagala aliwataka washiriki kuja na mapendekezo yenye tija katika usimamizi wa maafa.

 “Kongamano hili limekusudiwa kuwa jukwaa muhimu la kubadilishana uzoefu, kujadili changamoto, na kutoa mapendekezo ya kuboresha mifumo ya kitaifa ya usimamizi wa maafa.

Alisisitiza kuwa:”Nitoe wito kwa washiriki wote kushiriki kikamilifu katika mijadala, kwa sababu michango yenu ni muhimu katika kuhakikisha tunapata mapendekezo yatakayokuwa na tija katika usimamizi wa maafa.

Vilevile aliwataka washiriki kutumia fursa hiyo kuimarisha ushirikiano na kubuni njia mpya za kuongeza ustahimilivu wa jamii zetu ili kupunguza athari za maafa na kulinda maisha na mali.

Brigedia Jenerali Ndagala aliwashukuru wadau wote wanaoendelea kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu katika juhudi za kujenga Taifa lenye ustahimilivu dhidi ya majanga.

Alisema mchango wao katika kupanga, kutekeleza, na kufuatilia mipango ya usimamizi wa maafa nchini umeendelea kuwa wa thamani kubwa.

Kwa upande wake, Inspector Damian Muheya kutoka Makao Makuu ya Jeshi la Zimamoto na Uokoaji amesema kuwa, ili kufanikisha ustahimilivu endelevu usio na maafa, ni muhimu jamii kushiriki kikamilifu katika hatua za kinga na tahadhari dhidi ya majanga.

Naye Mhadhiri Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) Dkt. Barnabas Msongaleli ameeleza Taasisi yao imeendelea kutoa mchango katika kuzalisha wataalam wa kada ya usimamizi wa maafa nchini ili kuwa na wabobezi wa eneo hili na kuendelea kuleta tija katika masuala ya menejimenti ya maafa. 

“UDOM tumeendelea kutoa elimu, tunaendesha shahada ya awali ya menejimenti ya vihatarishi vya maafa ( Bachelor of Disaster Risk Management). Pia tunafanya tafiti mbalimbali zinazohusu kupunguza au kuzuia vihatarishi  vya maafa. Na kutoa huduma kwa jamii kwa njia ya kuwafikia jamii kuwapa elimu ya vihatarishi vya maafa na namna bora ya kukabiliana na maafa kabla hayajatokea,” alisisitiza Dkt. Msongaleli.

=MWISHO=
Share:

VETA inavyokuza ujuzi wa vijana kwa kuwafundisha Teknolojia mpya ya utengenezaji magari yasiyotumia mafuta


Published from Blogger Prime Android App



Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App



Na Joyce Kasiki, MBEYA

CHUO  cha Ufundi Stadi (VETA) mkoa wa Mbeya kimeonesha ubunifu mkubwa katika teknolojia ya kisasa kwa kuja na mfumo wa mafunzo ya magari ya Hybrid yanayotumia mota za umeme, huku yakipunguza au kuondoa kabisa utegemezi wa mafuta. 

Teknolojia hiyo imewasilishwa katika maonesho ya Wiki ya Vijana kitaifa, yakionesha mwelekeo mpya wa VETA katika kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya teknolojia duniani.

Mwanafunzi Adam Akyoo kutoka VETA Mbeya ameleza kuwa, mashine hiyo ya Hybrid imeundwa kwa kutumia mota maalum inayoweza kuzalisha umeme na kusaidia gari kusafiri hata pasipo mafuta.

 "Faida kubwa ya mota hii ni kwamba inaweza kuendesha gari bila kutumia mafuta kabisa,inapunguza gharama za uendeshaji na kumrahisishia mtumiaji safari, hasa pale mafuta yanapokatika na sheli ipo mbali," amesema Adam.

Adam amehimiza vijana wa Kitanzania kutumia fursa zilizopo kupitia vyuo vya VETA ambavyo vinaendelea kuimarishwa na serikali ili kuwapa vijana ujuzi wa kujiajiri au hata kuajiri wenzao.

“Tuna 'mode' ya kujifunza kwa vitendo, kila mwanafunzi anapata nafasi ya kujua teknolojia inavyofanya kazi. VETA haitoi tu nadharia, bali inakuandaa kuwa mtaalamu wa kweli wa teknolojia ya kisasa,” ameongeza.

Kwa mujibu wa Afisa Habari na Uhusiano wa VETA, David Mpondyo, teknolojia hiyo mpya ya magari ni sehemu ya juhudi za VETA kufundisha vijana ujuzi unaoendana na mahitaji ya soko la sasa.

 “Tuko kwenye maonesho ya Wiki ya Vijana tukionyesha kile ambacho vijana wanafundishwa kwenye vyuo vyetu. Si wote wanaofika vyuoni, lakini kupitia maadhimisho haya, wananchi wanaweza kuona na kuelewa kile kinachotolewa na VETA,” amesema Mpondyo.

Ameongeza kuwa VETA kwa sasa ina vyuo 80 ambapo kuna chuo katika kila mkoa, na kwamba ujenzi wa vyuo vingine 65 unaendelea katika kila wilaya nchini, juhudi zinazoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan ili kuongeza fursa za mafunzo ya ufundi stadi kwa wananchi wote.

Mpondyo amesema pia kuwa VETA imeamua kuandaa vijana kwa ajili ya teknolojia ya magari ya umeme kwa kuwa magari hayo sasa yameanza kuingia kwa kasi nchini. 

“Awali magari yote yalikuwa ya dizeli au petroli, lakini leo magari mengi yanatumia umeme,wateja wakipeleka magari hayo gereji, mafundi wengi wanayaharibu kwa sababu hawana ujuzi huo,ndiyo maana VETA imeamua kufundisha mfumo huu mpya kupitia 'mode' za kisasa,” amefafanua.

Mpondyo amesema, VETA inaendelea kuwa chachu ya maendeleo ya teknolojia na ujuzi nchini, ikiwapa vijana wa Kitanzania fursa ya kuendana na mabadiliko ya dunia na kuwa sehemu ya nguvu kazi yenye maarifa  yanayoendana na wakati .

.

Share:

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Labels

Recent Posts

Unordered List

  • Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  • Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  • Vestibulum auctor dapibus neque.

Pages

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.