RAIS SAMIA ATOA MAELEKEZO KWA JESHI LA POLISI


Published from Blogger Prime Android App


Na Joyce Kasiki,DODOMA

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amelitaka  Jeshi la PolisiNchini kkuongeza nguvu katika kukomesha matukio ya watu kupotea nchini.

Rais Dkt.Samia ameyasema hayo Bungeni Jijini Dodoma , Leo Juni 27,2025 wakati akihitimisha rasmi Bunge la 12 

Amesema kuwa pamoja na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitano ya Bunge hilo, bado yapo mambo yanayohitaji kushughulikiwa kwa dharura, likiwemo suala la usalama wa raia, hasa katika matukio ya watu kutoweka bila maelezo.

"Jeshi la Polisi lina wajibu wa kuhakikisha usalama wa wananchi, na mojawapo ya vipaumbele vyake sasa ni kuhakikisha kuwa matukio ya watu kupotea yanakomeshwa kabisa,” alisisitiza Rais Dkt. Samia
Share:

RAIS DKT. SAMIA AZUNGUMZA WAKATI WA KULIFUNGA BUNGE LA 12: "WABUNGE MMETIMIZA WAJIBU WENU KWA WELEDI NA UZALENDO"


Published from Blogger Prime Android App



Na Joyce Kasiki,DODOMA

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amelihutubia Bunge la Kumi na Mbili katika hafla ya kulifunga rasmi, huku akilipongeza Bunge hilo kwa kazi kubwa na nzuri ya kutunga sheria, kuisimamia serikali, na kuwakilisha wananchi kwa weledi na uzalendo mkubwa.

Akizungumza ndani ya Ukumbi wa Bunge jijini Dodoma, Rais Samia alimpongeza Mheshimiwa Spika Dkt. Tulia Ackson kwa kuliongoza Bunge kwa umahiri mkubwa, licha ya changamoto zinazotokana na tofauti za kisiasa na mitazamo ya wabunge mbalimbali.

"Mheshimiwa Spika, kuliongoza Bunge si kazi rahisi. Kwenye wengi kunamengi, lakini kwa umahiri wako na weledi, umeweza kuivusha mashua yetu salama hadi bandari, kama manahodha mahiri wa baharini,” alisema Rais Samia huku akishangiliwa na wabunge.

Rais Samia pia alitambua mafanikio ya kihistoria ya Spika Dkt. Tulia Ackson kwa kuwa mwanamke wa kwanza barani Afrika kushika nafasi ya Urais wa Mabunge ya Afrika (PAP), akisema mafanikio hayo yameongeza heshima ya Tanzania kimataifa.

Katika hotuba yake, Rais aliwapongeza wabunge wote kwa kutekeleza majukumu yao kikamilifu na kushiriki kikamilifu katika kujadili sera na mipango ya maendeleo ya taifa. Alisema kuwa Bunge hilo limekuwa na mchango mkubwa katika kujenga ustawi wa wananchi na kuleta maendeleo ya kweli.

"Nitumie fursa hii kulitushukuru Bunge kwa tuzo mlionipatia. Ninathamini kwa dhati kutambua kwenu mchango wangu katika maendeleo na ustawi wa nchi yetu,” alisema Rais.

Share:

WANANCHI SHINYANGA WAOMBA KUONGEZEWA SIKU ZA MADAKTARI BINGWA WA SAMIA

 

Published from Blogger Prime Android App



Na WAF, Shinyanga 

Wananchi mkoani Shinyanga wameomba kama kuna uwezekano wa kuongezwa siku za Madaktari Bingwa na Bobezi wa Rais Samia ili changamoto za Afya zinazowakabili ziweze kutatuliwa.

Hali hiyo imejitokeza Juni 25, 2025 ikiwa ni siku tatu tu, tangu kuanza kwa kambi ya madaktari bingwa wa Rais Samia  mkoani hapo. 

"Hatujui kwa wingi wetu huu kama kweli hizi siku sita zilizopangwa kama zitatutosha kama unavyoweza kuona Umati huu wa watu waliokuja kupata huduma za kibingwa," amesema Mzee John Mandu mkazi wa Chamaguha mkoani Shinyanga.

Kwa uoande wake Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo ya Manispaa Dkt. Moshi Ryioba amesema kumekuwa na ongezeko la idadi ya watu ikilinganishwa na siku zingine ambazo hazikuwa na Madaktari Bingwa.

"Tumepokea wananchi waliokuja kwa siku moja 167, hii sio hali ya kawaida kwani idadi ya kawaida huwa ni watu kati ya 50 hadi 70  kwa siku za kawaida," amesema Dkt. Ryioba.

Kwa upande wake Daktari Bingwa wa Upasuaji Dkt. Boazi Mwasambili kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda Mbeya, amekiri kupata ushirikiano wa kutosha kutoka kwa wenyeji wake na kufanikisha Operesheni mbili huku akijiandaa kufanya zingine nne (4). 

"Kama unavyoweza kuona hapa nipo na wataalam wawili, ambao tumekuwa nao bega kwa bega tangu siku ya kwanza kuna siku tulitoka hapa karibu saa mbili za usiku lakini hawajaacha kunipatia ushirikiano wakutosha," amesema Dkt. Mwasambili. 

Madaktari Bingwa walioweka kambi katika Hospitali ya Manispaa ya Shinyanga ni pamoja na Daktari bingwa Watoto, Wanawake, Upasuaji, Pua, Koo na Sikio, Magonjwa ya ndani, Meno pamoja na Wauguzi Mabingwa.
Share:

Waziri Jenista Mhagama: Mkataba wa Huduma Bora kwa Wateja kuchochea huduma bora




Published from Blogger Prime Android App




Joyce Kasiki,DODOMA

Waziri wa Afya, Jenista Mhagama, amezindua rasmi Mkataba wa Huduma Bora kwa Wateja, hatua inayolenga kuboresha utoaji wa huduma za afya na kuongeza uwajibikaji miongoni mwa watoa huduma katika vituo vyote vya afya nchini.

Akizungumza leo, Juni 25, 2025 jijini Dodoma katika hafla fupi ya uzinduzi wa mkataba huo, Waziri Mhagama ameagiza utekelezaji wake ufanyike kwa haraka na kwa ufanisi katika ngazi zote — kuanzia zahanati hadi hospitali za rufaa, taasisi na vituo vya afya binafsi.

"Ndani ya muda mfupi sana, nataka kuona kila kituo cha afya nchini kikiwa kimekamilisha mkataba huu. Hii ni pamoja na Zahanati, Vituo vya Afya, Hospitali za Wilaya, Rufaa za Mikoa na Kanda, pamoja na Taasisi zote za afya,” amesema Waziri Mhagama.

Aidha, amesisitiza kuwa mkataba huo si tu utakaoainisha haki na wajibu wa watoa huduma na wagonjwa, bali pia utatoa mwongozo wa gharama na viwango vinavyopaswa kuzingatiwa ili kuhakikisha huduma bora, za haki, na zenye uwiano sawa.

Waziri Mhagama amesema mkataba huo pia utawezesha utoaji wa taarifa muhimu kwa wagonjwa kabla ya matibabu, jambo linalojenga imani na kuondoa sintofahamu.

"Ni matarajio yangu kuwa kupitia mkataba huu, kila mmoja atatimiza wajibu wake. Hii itasaidia kupunguza malalamiko yasiyo ya lazima na kuifikisha sekta ya afya pale ambapo Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anataka ifike,” ameongeza.

Katika hotuba yake, Waziri huyo pia amepongeza juhudi za Rais Samia katika kuimarisha sekta ya afya kwa kuwekeza katika mafunzo ya wataalamu wa afya, ununuzi wa vifaa tiba vya kisasa kama MRI, PET-Scan na mashine za X-Ray — vifaa ambavyo amesema ni adimu hata kwa baadhi ya mataifa mengine.

Aidha, amesema mkataba huo unaendana na dira ya Wizara ya Afya ya kujenga jamii yenye ustawi bora inayochangia kikamilifu maendeleo ya taifa, sambamba na dhima ya utoaji wa huduma bora za afya kwa wote.

"Kazi kubwa tuliyobakiwa nayo sasa ni kuhakikisha kila Mtanzania anapata huduma bora bila kikwazo cha fedha. Tumeshatekeleza bima ya afya kwa wote, sasa tunalenga kuhakikisha fedha za kuendeleza huduma zinapatikana ili tuendelee kuwekeza zaidi,” amesema.

Pamoja na hayo, mkataba huo umeainisha huduma zitakazotolewa ikiwa ni pamoja na ushauri wa kitaalamu wa masuala ya afya, huduma za chanjo, utoaji wa vyeti vya usajili wa kitaaluma, leseni na vibali, pamoja na taarifa mbalimbali za sekta ya afya.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Seif Shekalage, amesema mkataba huo utaimarisha zaidi utendaji kazi na kuongeza uwajibikaji miongoni mwa watumishi wa sekta hiyo.


Share:

Waziri Mkuu Majaliwa azindua Mfumo wa kubadilisha taarifa

Published from Blogger Prime Android App
Published from Blogger Prime Android App


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb), akizindua rasmi Mfumo wa Kubadilishana Taarifa Serikalini (Government Enterprise Service Bus - GovESB) kwa kutumia kishkwambi, katika kilele cha Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma mwaka 2025, katika viwanja vya Chinangali jijini Dodoma.


Mfumo wa GovESB umesanifiwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao(e-GA) ikiwa ni utekelezaji wa maelekezo ya Rais wa Tanzania Mh.Dkt.Samia Suluhu Hassan na Sheria ya Serikali Mtandao Namba 10, ya mwaka 2019, ya kuhakikisha mifumo yote ya taasisi za umma inasoma na kubadilishana taarifa, ili kuboresha huduma kwa wananchi.



Published from Blogger Prime Android App
Share:

DktJafo aeleza mafanikio makubwa kiuchumi kupitia sekta ya viwanda

 





Na Mwandishi wetu,Dodoma


WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo, amewasilisha hotuba ya bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2025/2026 mbele ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo ametaja mafanikio makubwa na mikakati kabambe inayolenga kukuza uchumi wa viwanda na biashara nchini.

 

Aidha hotuba ya Waziri Jafo imeonesha mwelekeo chanya wa ukuaji wa sekta ya viwanda na biashara nchini ambapo kupitia bajeti aliyoiwasilisha amesema, serikali inaendelea kujenga msingi wa uchumi wa viwanda unaoendeshwa na ubunifu, ushindani, na uendelevu wa masoko ya ndani na nje.


Akisoma hotuba hiyo Bungeni jijini Dodoma, Dkt. Jafo ameliomba Bunge kuidhinisha jumla ya shilingi 135.8 bilioni kwa ajili ya kutekeleza majukumu ya wizara ambapo kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 93.9 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida huku shilingi bilioni 41.9 zikitengwa kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.

 

Amesema kuwa  sehemu kubwa ya matumizi ya kawaida ni mishahara ya wafanyakazi, inayofikia shilingi bilioni 75.8, huku bilioni 18.1 zikitengwa kwa matumizi mengineyo.

 

Jafo ametaja vipaumbele vya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2025/2026 kuwa ni pamoja na  kuendeleza Viwanda, Masoko, na Maendeleo ya Watu.

 

Kwa mujibu wa waziri huyo , katika mwaka ujao, wizara yake imepanga kuendeleza juhudi za kuimarisha sekta ya viwanda kwa kuwezesha uanzishwaji wa viwanda vipya, kuendeleza viwanda vya kimkakati, na kujenga miundombinu ya viwanda vidogo na vya kati (industrial clusters).

 

Aidha, amesema kuwa wizara itaendelea kuboresha mazingira ya biashara na kuvutia uwekezaji, kuimarisha upatikanaji wa masoko ya bidhaa za Tanzania ndani na nje ya nchi, pamoja na kusimamia ubora na usalama wa bidhaa ikiwemo chakula na vipodozi.

 

Kuhusu  uwanja wa biashara, wizara imepanga kuendeleza jitihada za kufungua masoko mapya, kurasimisha biashara mipakani, na kufanya utafutaji wa masoko  ili kusaidia wafanyabiashara kufikia fursa zinazojitokeza.

 

Mauzo ya Bidhaa yavunja rekodi

 

Dkt.Jafo amesema,katika miaka minne iliyopita, Tanzania imepiga hatua kubwa katika mauzo ya bidhaa nje ya nchi ambapo alisema,

Mauzo katika soko la SADC yaliongezeka kwa asilimia 127.7, kutoka dola milioni 1,303.4 mwaka 2021 hadi dola milioni 2,968 mwaka 2024.

 

Katika soko la Afrika Mashariki (EAC) amesema, mauzo yalipanda kutoka dola milioni 1,161.2 hadi 1,163.8 mwaka 2024 huku jumla ya mauzo katika bara la Afrika yamefikia dola milioni 3,946.76 mwaka 2024, ikiwa ni ongezeko la asilimia 61.2 tangu mwaka 2021.

 

Ametaja bidhaa zilizochangia ongezeko hilo ni pamoja na madini, pamba, kahawa, parachichi, saruji, sabuni, na bidhaa za kilimo.

 

AfCFTA: Tanzania yapanua wigo wa Biashara Afrika

 

Kwa mujibu wa Waziri Jafo, Tanzania imekuwa miongoni mwa nchi zinazofaidika na Soko la Biashara Huru la Afrika (AfCFTA), ambapo hadi Machi 2025 nchi imefanikiwa kusafirisha bidhaa kwenda mataifa 18 ya Afrika kwa kutumia vyeti vya uasili wa bidhaa. Bidhaa hizo ni pamoja na nyuzi za mkonge, vioo, kahawa na mchele.

 

Soko la Kimataifa: Marekani na Umoja wa Ulaya

 

Waziri Jafo pia alieleza mafanikio ya Tanzania katika soko la Marekani kupitia mpango wa AGOA, ambapo mauzo yameongezeka kutoka dola milioni 33.06 mwaka 2021 hadi dola milioni 85.4 mwaka 2023 – sawa na ongezeko la asilimia 158.3. Bidhaa maarufu zilizouzwa ni nguo, kahawa na mbogamboga.

 

Kwa upande wa Umoja wa Ulaya (EU), mauzo yameongezeka kwa asilimia 38.5, kutoka dola milioni 891.5 mwaka 2021 hadi dola milioni 1,234.3 mwaka 2024. Bidhaa zilizouzwa ni pamoja na mazao ya chakula, madini, maua, na ngozi.

 

Vikwazo vya Biashara: Serikali Yashughulikia Changamoto

 

Katika juhudi za kuvutia biashara zaidi, serikali imefanikiwa kutatua jumla ya vikwazo vya kibiashara 70 kati ya Tanzania na nchi jirani, vikiwemo Kenya na Zambia. 


Kwa mujibu wa Waziri Jafo,hatua hiyo imesaidia kurahisisha biashara mipakani na kuongeza ushirikiano wa kiuchumi kikanda.

 


Share:

Kapinga amtilia shaka MF Contractor






Published from Blogger Prime Android App



Na Joyce Kasiki,DODOMA


NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amemuelekeza Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kukutana na Mkandarasi MF anayetekeleza mradi wa umeme katika vijiji 15 vya Wilaya ya Nyasa, ili kuangalia uwezekano wa kuteua wakandarasi wadogo (sub-contractors) kutokana na udhaifu wa mkandarasi huyo katika utekelezaji wa kazi.

Kapinga alitoa maelekezo hayo kufuatia swali la nyongeza lililoulizwa Bungeni jijini Dodoma Aprili 24,2025 na Mbunge wa Nyasa, Mhandisi Stella Manyanya, ambaye alitaka wakandarasi waondolewe kutokana na kutokuwepo kwa maendeleo yoyote ya kazi katika maeneo husika.

"Pamoja na pongezi kwa Wizara ya Nishati, lakini kwa kuwa vitongoji vyote vilivyopangiwa kupata umeme awamu hii kupitia wakandarasi MF na Triple C (CCC), hakuna hata kimoja kilichowashiwa umeme. Kwa nini wasiondolewe na kuwekwa wakandarasi wenye uwezo?" alihoji Manyanya.

Akijibu hoja hiyo, Naibu Waziri Kapinga alifafanua kuwa mkandarasi anayetekeleza mradi wa vitongoji hivyo ni kampuni ya CCC na alimtaja kuwa ni mkandarasi mzuri, ambaye kwa sasa yupo katika hatua za manunuzi na atatembelea eneo la mradi hivi karibuni.

Hata hivyo, kuhusu Mkandarasi MF, Kapinga alisema:
"Namuelekeza Mkurugenzi Mkuu wa REA, na tayari tulishazungumza, afanye utaratibu wa kukutana naye ili watafute 'sub-contractors' kwa sababu uwezo wake tayari unatia mashaka. Tutasimamia hili kwa karibu ili kuhakikisha kuwa mradi unakamilika kwa wakati." alisisitiza Kapinga.



Share:

Serikali yaombwa kupeleka maji Tukuyu Kutoka Ziwa Nyasa




Published from Blogger Prime Android App



DODOMA

MBUNGE wa Viti Maalum Sophia Mwakagenda ameiomba Serikali kupeleka maji Mji wa Tukuyu Kutoka Ziwa Nyasa Ili kusaidia wananchi wa wilaya hiyo kupata maji safi na salama.

Akiuliza swali la nyongeza Bungeni jijini Dodoma Mwakagenda amesema  Mji wa Tukuyu hauna maji huku alihoji lini Serikali itapeleka fedha ili kujenga mradi wa kutoa maji Ziwa Nyasa na kuyafikisha Mji wa Tukuyu.

"Kama ilivyo kwa ziwa Victoria, tuna Ziwa Nyasa na Mji wa Tukuyu hauna maji, ni lini Serikali italeta fedha kuhakikisha maji yanatoka Ziwa Nyasa Hadi kufika  Tukuyu?

Akijibu swali hilo Waziri wa Maji Jumaa Aweso amesema Moja ya mikakati iliyopo Serikalini ni kuhakikisha rasilimali zilizopo nchini zinatumika na kutatua changamoto za wananchi.

"Nimhakikishie Mheshimiwa  Mbunge kwamba Moja ya mikakati na maelekezo ni kuhakikisha rasilimali zilizopo nchini zinatumika na kutatua matatizo ya maji,kwa  hiyo maeneo ya Ziwa Nyasa ni moja ya mikakati ya Wizara ,na Wizara ipo katika hatua mbalimbali kufanya 'visibility Study' ,naamini wananchi wa maeneo hayo pia watanufaika kupata Huduma ya maji safi na salama."amesisitiza Aweso
Share:

Sekiboko ahoji mkakati wa Serikali kuboresha soko la machungwa Tanga




Published from Blogger Prime Android App



MBUNGE wa Viti Maalum Husna Sekiboko amehoji hatua zinazochukukiwa na Serikali Ili kulinda Kilimo Cha matunda kwa lengo lai kuokoa soko la matunda linalosuasua kutokana na uingizaji mkubwa wa matunda nchini.

Akiuliza swali Bungeni Sekiboko pia amesema "Mkoa wa Tanga ni maarufu kwa Kilimo cha matunda hasa machungwa lakini bado hayajapati soko zuri kwenye viwanda,ni upi mkakatii wa Serikali katika kuboresha Kilimo Cha matunda ili kuweza kukidhi mahitaji ya viwandani?amehoji Sekiboko na kuongeza kuwa 

"Pamekuwa na changamoto kubwa ya kuoza matunda kabla ya kufika sokoni ,ni upi mkakati wa Serikali wa kujenga vyumba baridi kwa ajili ya kuhifadhi matunda ."

Akijibu maswali hayo ,Naibu Waziri wa Kilimo David Silinde amesema katika  kulinda soko na kudhibiti uingiaji holela wa matunda nchini, Serikali imechukua hatua mbalimbali zikiwemo kuanzisha Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) ambayo itaweka utaratibu wa kuwezesha uingizaji na usafirishaji nje wa mazao ya nafaka na mazao mchanganyiko yakiwemo matunda.

"Pia imeamasisha uanzishaji wa viwanda vya kusindika matunda ili kuimarisha soko la ndani na kupunguza upotevu,kutoa ruzuku ya pembejeo kwa mazao ya matunda ikiwemo maembe, machungwa na parachichi ili kuongeza tija na kuimarisha utafiti na uzalishaji wa mbegu na miche bora ya matunda kulingana na mahitaji ya soko.

 Aidha Silinde amemthibitishia Mbunge huyo kwamba Serikali, inatambua mkoa wa Tanga ni Moja ya Mkoa unaotegemewa  kwa Kilimo cha machungwa .

"Tunakiri kwamba kuna changamoto kubwa ya kuoza kwa matunda hayo ambayo imekuwa ni Moja ya jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali kuokoa matunda hayo ambapo kazi kubwa iliyofanyika sasa hivi ni kuhamasisha sekta Binafsi kuingia katika kujenga viwanda vidogo vidogo kwa ajili ya kuongeza thamani ya mazao haya kama vile Kutoka katika tunda kuwa juisi  na Tanga ndio mkoa ambao sasa hivi tumeuweka kwenye mkakati huo."amesema Silinde

Kuhusu kuoza mazao amesema,Serikali inao Mpango madhubuti na tayari  imepata fedha kwa ajili ya kujenga vyumba baridi kwa ajili ya kuhifadhi haya matunda
Share:

Tanzania ilivyojidhatiti maonesho ya Expo 2025 Osaka,Japan






Published from Blogger Prime Android App



Na Joyce Kasiki,DODOMA

WAZIRI  wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jaffo, amesema kuwa Tanzania imejipanga kushiriki kikamilifu katika Maonesho ya Dunia ya EXPO 2025 yatakayofanyika mjini Osaka, Japan kuanzia Aprili 12 hadi Oktoba 13, 2025 kwa lengo la kutangaza fursa za biashara, uwekezaji, utalii, pamoja na Mila na Utamaduni wa Taifa.

Akizungumza leo jijini Dodoma na waandishi wa habari, Dkt. Jaffo amesema EXPO ni maonesho makubwa ya kimataifa yanayoratibiwa na Bureau of International Exposition (BIE) ambapo nchi wanachama, ikiwemo Tanzania, hupiga kura kuchagua mwenyeji wa maonesho hayo.

“TanTrade kwa niaba ya Serikali ya Tanzania, imekuwa ikiratibu ushiriki wa nchi yetu kwenye EXPO tangu mwaka 1967. Hadi sasa tumeshiriki katika EXPO takriban tisa, ikiwemo Expo 2020 Dubai na Expo ’70 Japan. Ushiriki huu umekuwa jukwaa muhimu la kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi,” alisema Waziri Jaffo.

EXPO 2025 Osaka inabeba kauli mbiu kuu isemayo “Kuwezesha jamii kwa Maisha Endelevu” ambapo Tanzania imechagua kaulimbiu ndogo ya “Kuunganisha Maisha – Connecting Lives” yenye malengo ya kuunganisha uzalishaji wa ndani na masoko ya nje, kuhamasisha uwekezaji, kuimarisha mawasiliano ya kiteknolojia, na kuchochea sekta ya utalii.

Dkt. Jaffo amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi zaidi ya 160 zilizothibitisha ushiriki wake rasmi, na kwamba banda la Tanzania litakuwa na ukubwa wa mita za mraba 53 kwa ajili ya maonesho na mita za mraba 15 kwa ajili ya biashara.

“Kwa Expo 2025 Osaka, tuna matarajio makubwa zaidi. Tunaamini tutaongeza upatikanaji wa masoko ya bidhaa za Tanzania, kuimarisha uchumi wa nchi, na kuvutia wawekezaji wa kimkakati kupitia ushirikiano na sekta binafsi,” amesema Dkt. Jaffo.

Amesema maonesho hayo pia yataambatana na programu maalum za kila wiki, ikiwemo Utalii, Miundombinu, Kilimo na Uchumi wa Buluu, Afya, Sanaa na Utamaduni, Nishati na Sayansi na Teknolojia. Kila programu itaratibiwa na Wizara husika kwa kushirikiana na taasisi na sekta binafsi.

Aidha, Siku ya Tanzania katika EXPO hiyo imepangwa kufanyika Mei 25, 2025 ambapo mgeni rasmi atakuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa. Siku hiyo itafuatiwa na Kongamano la Biashara, Uwekezaji na Utalii litakalofanyika Mei 26, 2025.

Waziri Jaffo alitoa wito kwa taasisi za umma, mashirika ya kimataifa na binafsi kushiriki kikamilifu katika maandalizi na maonesho hayo kwa kuwasilisha maudhui ya miradi ya kimkakati, kuthibitisha ushiriki katika programu na kongamano, pamoja na kuandaa mapendekezo ya maeneo ya ushirikiano na taasisi za Kijapani.

“Washiriki wote wanatakiwa kujisajili kupitia tovuti ya TANTRADE au kwa kutumia QR code inayotangazwa kupitia vyombo vya habari,” alihitimisha.

EXPO 2025 Osaka ni fursa adhimu kwa Tanzania kuonesha dunia nguvu yake ya kiuchumi, vivutio vyake vya kiutalii, pamoja na uwezo wake mkubwa katika ubunifu, teknolojia na maendeleo ya jamii.
Share:

Rais Samia aitaka Mahakama kutenda haki bila kuangalia hali ya mtu




Published from Blogger Prime Android App


Na Mwandishi wetu, DODOMA 

RAIS Dkt.Samia Suluhu Hassan amewataka watendaji wa Mahakama kuhakikisha kasi ya utoaji haki kwa wananchi inaendana na ubora wa jengo jipya  la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania ambalo limejengwa kwa maslahi mapana ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

Dkt.Samia ametoa kauli hiyo wakati wa hafla ya uzinduzi wa jengo hilo  sambamba na jengo la Utumishi wa Mahakama na Makazi ya Majaji ambayo yote kwa pamoja yamegharimu kiasi Cha shilingi bilioni 185.4.

Amesema kuwa na majengo mazuri ni kwa ajili ya kujenga mazingira mazuri ya utendaji kazi hasa ya utoaji haki kwa wananchi.

Dkt.Samia amesema,mazingira hayo mazuri yaendane na ubora wa huduma zinazotolewa katika majengo hayo .

Amesema ,Serikali imefanya kazi kubwa ya kujenga mazingira mazuri ya utendaji kazi kwa Majaji hapa nchini na kuwataka nao kufanya kazi ya utoaji haki bila kuangalia Hali ya mtu.

Aidha Dkt Samia ameipongeza Mahakama kwa  ujenzi wa jengo hilo  ambalo limezingatia matumizi ya TEHAMA huku akionyesha kufurahishwa na Mifumo ya Mahakama kusomana.

Amesema ,Mifumo hiyo inamwezesha mtu kuangalia mwenendo wa kesi katika mkoa wowote anaoutaka.

Ametumia nafasi hiyo kuhimiza Mahakama kuendelea kuifanya Mifumo yake kusomana Ili kurahisisha kazi ya utoaji haki na kupunguza mrundikano wa kesi mahakamani.

Amesema,kwa upande wa Serikali imeendelea kuongeza bajeti ya Mahakama Kila mwaka Kutoka bilioni 161 Hadi shilingi bilioni 321 mwaka huu wa fedha kwa lengo la kurahisisha utendaji kazi wa Mahakama.

Kwa upande wake Jaji Mkuu wa Tanzania Prof.Ibrahim Hamis Juma ameishukuru Serikali kwa kuiwezesha Mahakama kupata jengo hilo zuri na hivyo Makao Makuu ya Mahakama kuhamia Dodoma.

"Tunashukuru mheshimiwa Rais kwa kuiwezesha Mahakama kufanya maboresho kupitia mipango yake  ,bila uwezeshaji mipango yetu ingebaki kwenye makaratasi."alisema Prof.Ibrahim

Share:

Wizara ya Habari Ndiyo Roho ya Nchi - Mhe. Abdulla



Published from Blogger Prime Android App


Na Adelina Johnbosco - MAELEZO

Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, amesema Wizara ya Habari  ni muhimu sana katika nchi kutokana na majukumu yake ya uhabarishaji wa masuala mbalimbali katika kila nyanja ndani na nje ya Tanzania. 

Amesema hayo leo Aprili 3, 2025 katika Hoteli ya New Amaan Zanzibar wakati akifungua Kikao Kazi cha 20 cha Maafisa Habari wa Serikali kitakachodumu hadi Aprili 6, 2025.

"Wizara ya Habari ina mambo mengi, na ndiyo roho ya nchi, wengine wanasema ni Wizara ya Fedha, lakini hata fedha zenyewe zinataka habari, unaweza kuwa nazo ukazitumia lakini bila ya habari zisionekane matumizi yake" amesisitiza Mhe. Abdulla 

Vile vile, amewashukuru Maafisa Habari kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kutekeleza majukumu yao ya kuuhabarisha umma na ulimwengu kwa ujumla kuhusu mafanikio ya Serikali.

"Kazi yenu Maafisa Habari imetukuka, imeifanya Tanzania kupata sifa kubwa, dunia inaendelea kupata habari za Tanzania, kuijua miradi yake hasa utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)" ameongeza Mhe. Abdulla

Sanjari na hayo, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, amewataka walengwa wa Kikao Kazi hicho ambao ni Maafisa Habari wa Serikali nchi nzima, kuzitumia mada mafunzo zitakazowasilishwa ili kufanya kazi kwa utaalam na si kufanya kazi kwa mazoea.

..............Mwisho..........






Share:

Maafisa Habari, Kikao Kazi Hiki ni cha Mafundo na Mazingativu - Msigwa

Published from Blogger Prime Android App




Na Adelina Johnbosco - MAELEZO

Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo ambaye pia ni Msemaji Mkuu wa Serikali, Bw. Gerson Msigwa, amewataka Maafisa Habari wa Serikali kutambua kwamba, ujio wao Zanzibar katika Kikao Kazi ni kwa ajili ya kufundwa na kuzingatia yote yatakayoelekezwa na kukumbushwa juu ya utekelezajiwa majukumu yao.

Bw. Msigwa ametanabahisha hayo wakati wa ufunguzi wa Kikao Kazi cha 20 cha Maafisa Habari wa Serikali kinachofanyika katika Hoteli ya New Amaan Zanzibar, leo Aprili 3, 2025.

"Hiki ni kikao cha mafundo na mazingativu, tunafundana na kuzingatia mafundo kwa Maafisa Habari, Mawasiliano, Uhusiano na Itifaki wa Serikali" amesisitiza Bw. Msigwa

Aidha, ametaja malengo ya Kikao Kazi hicho kwa Maafisa Habari wa Serikali kuwa ni kuimarisha mawasiliano ya Serikali kwa umma kupitia programu za kujenga uwezo kwa watumishi pia kuimarisha Muungano na kubadilishana uzoefu.

Kwa upande wake Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar, Mhe. Tabia Maulid Mwita, ameshukuru kukubaliwa ombi lake la Kikao Kazi hicho kufanyika Zanzibar na kutaja sababu kuu ya kufanya hivyo ikiwemo Maafisa Habari kujionea shughuli mbalimbali za utalii, michezo na maendeleo makubwa ndani ya Zanzibar. 

"Lengo kubwa la kuomba Kikao Kazi hiki kufanyika Zanzibar ni kuendelea kuimarisha Muungano wetu, pili ni kuwawezesha Maafisa Habari kuja kuiona Zanzibar ya sasa ya Dkt. Hussein Ali Mwinyi, hivyo watapata kibali cha kuisemea Zanzibar kule Tanzania Bara na duniani kote" - Mhe. Tabia

Vile vile ameahidi kwamba, Wizara yake ya Habari Tanzania Zanzibar itaendelea kushirikiana na Wizara ya Habari Tanzania Bara katika nyanja zote zinazohusu sekta ya Habari nchini.

Wakati mafundo hayo yakiendelea, kikao hicho kimetoa fursa ya upimaji wa afya bure kwa wadau wote wa habari wanaoshiriki kikao hicho na wananchi watakaofika katika viwanja vya Hoteli ya New Amaan ambapo madaktari bingwa kutoka Hospitali ya Taifa Muhimbili, MOI, JKCI na Lumumba wanaendelea kutoa huduma za afya za kibingwa kuanzia leo Aprili 3, 2025 hadi ukomo wa kikao hicho Aprili 6, 2025.

...........Mwisho.......






Share:

Wahitimu kidato cha nne waaswa kubadilisha Tahasusi kabla ya muhula wa masomo 2025 kuanza


Published from Blogger Prime Android App







Published from Blogger Prime Android App

Published from Blogger Prime Android App



Na Mwandishi Wetu,Dodoma

WAZIRI wa Nchi,Ofisi ya Rais ,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mohamed Mchengerwa,amewataka wahitimu wa kidato Cha nne  kwa mwaka 2024 ,kufanya mabadiliko ya tahasusi (combination) kulingana na ufaulu wao utakaowawezesha kuoangiwa kidato Cha Tano na vyuo kwa mwaka 2025.

Amesema zoezi hilo la kubadili tahasusi limeanza Machi 31 na litafunhwa  April 31 mwaka huu .

Mchengerwa ameyasema hayo  jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu taarifa kwa wahitimu wa kidato Cha mwaka 2024 kufanya mabadiliko ya tahasusi za kidato Cha Tano na kozi za vyuo kwa njia ya mtandao kwenye mfumo wa Uchaguzi wa wanafunzi wa kidato Cha Tano na vyuo mwaka 2025.

"Leo nimewaita hapa kwa ajili ya kutoa taarifa muhimu kwa wahitimu wa Kidato cha Nne mwaka 2024 kuhusu fursa ya kubadilisha machaguo ya Tahasusi za Kidato cha Tano na Vyuo vya Kati na Elimu ya Ufundi kwenye mfumo wa kielektroniki wa uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga na Kidato cha Tano na Vyuo."amesema Mchengerwa

Amesema hayo ni  maandalizi ya awali ya uchaguzi wa wanafunzi watakaojiunga Kidato cha Tano na Vyuo vya Serikali Mwaka, 2025. 

Waziri Mchengerwa alisema, Serikali imekuwa ikitoa fursa kwa wahitimu wa Kidato cha Nne kufanya mabadiliko ya machaguo ya Tahasusi (combination) na Kozi mbalimbali walizozichagua kupitia Fomu ya Uchaguzi .

Amesema,fursa hiyo huwawezesha wanafunzi kurekebisha machaguo yao kulingana na ufaulu waliopata kwenye matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne yaliyotangazwa na Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA).

Aidha amesema,Serikali kupitia Ofisi ya Rais  TAMISEMI imekamilisha zoezi la awali la kuingiza kwenye kanzidata taarifa zilizo kwenye Fomu za Uchaguzi za wanafunzi kama zilivyojazwa na wanafunzi wakiwa shuleni. 

"Kukamilika kwa zoezi hili kunatoa fursa kwa wanafunzi kuweza kufanya mabadiliko ya machaguo/ tahasusi/ kozi kwa njia ya mtandao ambapo baada ya wanafunzi kufanya marekebisho yao, kanzidata hiyo ndiyo itakayotumika kuwachagua na kuwapangia nafasi za Kidato cha Tano na Kozi mbalimbali katika Vyuo vya Kati na vya Elimu ya Ufundi kwa kuzingatia sifa za ufaulu na machaguo yao. "Amesema

Amesema,Ofisi ya Rais  TAMISEMI inatoa fursa kwa wahitimu wa elimu ya sekondari Kidato cha Nne, mwaka 2024 kubadili machaguo yao ili kutoa nafasi zaidi kwa mwanafunzi kusoma tahasusi au kozi itakayomwandaa kuwa na utaalamu stahiki katika maisha yake ya baadaye. 

Kwa.mujibu wa Mchengerwa,zoezi hilo litatoa fursa zaidi ya wanafunzi kuongeza machaguo na kufanya machaguo mapya ya Tahasusi na Kozi.

Amewaasa   wazazi/ walezi kushiriki katika zoezi hili kwa kushauriana na watoto wao katika kufanya machaguo sahihi kulingana na ufaulu wao lakini pia,amewahimiza  wahitimu wote  kufanya marekebisho ya machaguo ya tahasusi na kozi kulingana na ufaulu wao, kwa kuingia kwenye Mfumo wa Uchaguzi wa Wanafunzi unaopatikana kupitia kiunganishi cha selform.tamisemi.go.tz

Aidha amesema,maelekezo kwa wahitimu na jinsi ya kufanya mabadiliko watayapata kwenye mfumo kupitia 'user manual' pamoja na video ya youtube zilizopo kwenye mfumo huo.

Amesema,ili kuingia kwenye mfumo  mhitimu anapasqa atumie Namba yake ya  Mtihani wa kuhitimu Kidato cha Nne mwaka 2024, Jina lake la Mwisho, Mwaka wa Kuzaliwa na Alama ya Ufaulu aliyopata kwenye somo atakaloulizwa na mfumo au swali lolote atakaloulizwa.

"Ni matumaini yangu kuwa wahitimu wote watatumia kwa ukamilifu fursa waliyopewa ya kubadilisha Tahasusi na Kozi kulingana na ufaulu waliopata na pia wataweza kusoma tahasusi/kozi ambazo wamefaulu vizuri ama wana malengo nazo zaidi. "

Waziri huyo amewasisitiza wasisitiza wanafunzi, wazazi/ walezi kutumia muda huo vyema ili kuepusha changamoto zinazoweza kujitokeza mara baada ya matokeo ya uchaguzi wa wanafunzi wa kujiunga na Kidato cha Tano na Vyuo kutangazwa huku akisema ni muhimu kuzingatia muda uliotolewa wa kufanya marekebisho ili ratiba ya kuwachagua na kuwapangia shule na vyuo iweze kuendelea kwa muda uliopangwa. 

Aidha ameema huduma hiyo ya kubadilisha tahasusi ni bure na endapo wanafunzi watapata changamoto, wawasiliane na Dawati la Huduma la Mteja kupitia barua pepe: huduma@tamisemi.go.tz au kuwasiliana moja kwa moja na Kituo cha Huduma kwa Wateja kwa simu +255 262 160 210 na +255 735 160 210. 

Aidha alisema, pamoja na maelekezo hayo, kwa mwanafunzi, mzazi/mlezi atakayekuwa na suala linalohitaji maelezo au ufafanuzi zaidi aende katika Ofisi za Elimu za Mikoa na Halmashauri.



Share:

Nderiananga aongoza ujumbe wa Tanzania katika mkutano wa tatu wa Kimataifa wa watu wenye ulemavu Ujerumani

Published from Blogger Prime Android App


Published from Blogger Prime Android App


Published from Blogger Prime Android App




NA. MWANDISHI WETU BERLIN – UJERUMANI


Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge na Uratibu Mheshimiwa Ummy Nderiananga ameongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania unaoshiriki Mkutano wa Tatu wa Kimataifa wa Watu wenye Ulemavu unaofanyika jijini Berlin, Ujerumani tarehe 2 hadi 3 April,2025. 

Mkutano huo umeandaliwa na Shirikisho la Kimataifa wa Watu Wenye Ulemavu (IDA), Serikali ya Ujerumani, na Serikali ya Jordan na kufunguliwa rasmi kwa pamoja na Kansela wa Ujerumani Mhe. Olaf Scholz na Mfalme Abdullah II wa Jordani.

Akizungumza wakati wa ufunguzi rasmi wa Mkutano huo Mhe. Scholz amesisitiza juu ya umuhimu wa kushirikiana kimataifa kukuza haki na ujumuishaji wa masuala ya Watu Wenye Ulemavu.

“Ushirikiano wa kimataifa ni nguzo muhimu katika kuhakikisha haki na ujumuishaji wa watu wenye ulemavu unatekelezwa kikamilifu duniani kote kwa kushirikiana, serikali, mashirika ya kimataifa, sekta binafsi, taasisi za elimu, mashirika ya kiraia, na Mashirika ya Watu Wenye Ulemavu tunaweza kuunda sera na mipango madhubuti inayohakikisha usawa wa fursa na ushiriki kamili wa watu wenye ulemavu katika jamii, “ alisisitiza.

Naye Mfalme Abdullah II wa Jordani akizungumza wakati wa ufunguzi wa Mkutano huo alisisitiza dhamira ya dhati ya kuendeleza haki na ujumuishaji wa watu wenye ulemavu.

Mfalme Abdullah II alitilia mkazo umuhimu wa ushirikiano wa kimataifa katika kuhakikisha fursa sawa na ushiriki kamili wa watu wenye ulemavu katika nyanja zote za jamii.

Mkutano huo unalenga kuhamasisha juhudi za kimataifa katika kufanikisha ujumuishaji wa watu wenye ulemavu duniani na kuwaleta pamoja wadau wa ngazi za juu kujadili na kushiriki maendeleo katika ujumuishaji wa watu wenye ulemavu, kutoka serikalini, mashirika ya kimataifa, sekta binafsi, taasisi za elimu ya juu, mashirika ya kiraia na mashirika ya watu wenye ulemavu kutoka nchi mbalimbali.

Mkutano wa Kimataifa wa Watu wenye Ulemavu (GDS) ni jukwaa la kipekee la kimataifa linaloangazia uboreshaji wa maisha ya watu wenye ulemavu, hususan kutoka Kusini mwa Dunia. 

Mkutano huo ulianzishwa mwaka 2017 kwa lengo la kuwakutanisha wadau wa kimataifa, kikanda, na kitaifa wanaoshiriki malengo na maono ya maendeleo jumuishi kwa watu wenye ulemavu na hatua za kibinadamu.

Mkutano huu unalenga kuziba pengo kati ya nyanja mbili za ujumuishaji watu wenye ulemavu na ushirikiano wa maendeleo.

Mkutano wa Kimataifa wa Watu wenye Ulemavu hufanyika kila baada ya miaka mitatu ni jukwaa linalohusisha utetezi wa mara kwa mara na wadau wa maendeleo ya wenye ulemavu kimataifa pamoja na kuhamasisha vuguvugu la haki za watu wenye ulemavu na washirika wake duniani.

Mkutano huo pia unaangalia namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya nchi wanachama na Mashirika ya Watu Wenye Ulemavu (OPDs) kupitia mipango ya pamoja ya uandaaji wa mkutano.




































Share:

UWT yalaani Mwenezi BAWACHA kushambuliwa


Published from Blogger Prime Android App


Na Joyce Kasiki,Dodoma
UMOJA  wa Wanawake wa  Chama cha Mapinduzi Taifa (UWT), umelaani shambulio la kudhuru mwili alilofanyiwa Mwenezi wa Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA), Sigilaga Mligo, ambalo limesababisha maumivu makali hadi kupelekea kulazwa hospitalini huku akishangazwa na uongozi wa CHADEMA Taifa kukalia kimya suala hilo.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Mwenyekiti wa UWT  Taifa Mary Chatanda amesema  kuwa shambulio hilo ni aina ya unyanyasaji, ukandamizaji, na uonevu dhidi ya mwanamke lakini pia na mfumo dume uliopo katika chama cha CHADEMA

Amesema kitendo hicho kinakwenda kinyuma na madhumuni ya UWT, kama inavyoelezwa katika kifungu (f) cha katiba yake, kinachotamka kuwa Umoja huo ni chombo cha ukombozi wa wanawake wa Tanzania dhidi ya unyanyasaji, unyonyaji, ukandamizaji, na mila zote zinazorudisha nyuma maendeleo ya wanawake.

UWT imeeleza masikitiko yake kuhusu mazingira ya tukio hilo, ambapo inadaiwa kuwa Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA, John Heche, alikuwepo lakini hakuchukua hatua yoyote.

Umoja huo umehoji ukimya wa viongozi wa Baraza la Wanawake la CHADEMA (BAWACHA) kuhusu shambulio hilo, hasa kwa kuwa mhanga ni kiongozi wa ngazi ya juu katika baraza hilo.

Kadhalika, UWT imeitaka Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa kufuatilia kwa karibu uanzishwaji wa madawati ya jinsia ndani ya vyama vya siasa, kama inavyotakiwa na Sheria ya Vyama vya Siasa ya mwaka 2023. Umoja huo unataka madawati hayo yawe na mamlaka na uwezo wa kuchukua hatua dhidi ya vitendo vya unyanyasaji, udhalilishaji, na ukandamizaji wa kijinsia katika siasa.

Katika hatua nyingine, UWT imewataka wanawake kujitokeza kwa wingi na kuchukua fomu za kugombea nafasi za uongozi pindi muda utakapofika, ikisisitiza kuwa uchaguzi wa mwaka huu ni wa kikatiba na unapaswa kuwa huru na wa haki.

UWT imetoa pole kwa Bi. Sigilaga Mligo na kumtakia uponyaji wa haraka, huku ikihimiza hatua madhubuti zichukuliwe dhidi ya wote waliohusika katika shambulio hilo.
Share:

SOS Children's Village yakabidhi Mwongozo wa Taifa wa Uanzishaji, Uendeshaji na Usimamizi wa makao ya watoto


Published from Blogger Prime Android App



Na WMJJWM- Dodoma 

KATIBU  Mkuu wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu amepokea ugeni kutoka  Shirika la Watoto la SOS Children's Village  ambapo ugeni huo ukiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo  Aisha Salim Ali leo Machi 27, 2025 katika Ofisi za Wizara jijini Dodoma.

Dkt Jingu amelipongeza Shirika hilo kwa jitihada zake za kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha  wanadhibiti changamoto ya watoto kuishi na kufanya kazi mitaani baada ya Shirika hilo kukabidhi Mwongozo wa Taifa wa Uanzishaji, Uendeshaji na Usimamizi wa makao ya watoto nchini.

Aidha Dkt. Jingu ametoa wito kwa jamii kuimarisha taasisi ya familia na kuepuka migogoro kwani tafiti zinaonesha hivi karibuni kumekua na kuvunjika kwa ndoa nyingi  na  kupelekea kupatikana kwa wimbi la watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la SOS Children's Village   Aisha Salim Ali ameahidi ushirikiano kati ya Shirika lake na Wizara katika kuhudumia Watoto katika Makao ya Watoto kwa kuweka namna nzuri ya Utoaji wa huduma na Malezi katika Makao hayo.

Mwisho.
Share:

RAIS SAMIA AFTURISHA WATOTO KIKOMBO DODOMA



Published from Blogger Prime Android App


Published from Blogger Prime Android App


Published from Blogger Prime Android App


 
Na WMJJWM- Dodoma 
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amewafuturisha Watoto wanaolelewa katika Makao ya Taifa ya Watoto Kikombo Dodoma katika Kipindi hiki cha mwezi Mtukufu wa Ramadhan.
 
Akizungumza wakati wa Iftari hiyo kwa niaba yake, Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mwanaidi Ali Khamis alitoa shukurani kwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuendelea kuweka mazingira wezeshi yenye lengo la kuondoa kabisa changamoto zinazowakabili watoto walio katika mazingira hatarishi. 

“Kipekee kabisa, ninamshukuru tena Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kufuturisha watoto wanaoishi katika Makao ya Taifa ya Watoto Kikombo pamoja na maeneo mengine ya nchi hususani Watoto wa Mkoa wa Arusha na Dar Es Salaam”. ameeleza Naibu Waziri Mwanaidi.

Aidha aliongeza kuwa Wizara inatambua na kuthamini mchango unaotolewa na wadau kwa lengo la kuhakikisha watoto walio katika mazingira hatarishi wanapatiwa huduma ya malezi ya muda mfupi katika Makao ya Watoto.

“Serikali na Wadau tutaendelea kushirikiana kutoa huduma kulingana na sheria, kanuni na miongozo tuliyojiwekea, nitumie fursa hii kuwaomba wamiliki wa makao ya kulelea watoto kuhakikisha mnatoa huduma kwa mtoto kwa kuzingatia maslahi mapana ya mtoto”. amesema Naibu Waziri Mwanaidi.

Mhe. Mwanaidi alitumia fursa hiyo kuwapongeza viongozi, walezi na watendaji wa Wizara kwa kuendelea kuratibu na kusimamia utekelezaji wa afua za malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto katika makao yote hapa nchini. 

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt.John Jingu amewasihi watoto waishio katika makao hayo kuishi kwa upendo na amani huku wakiweka bidii katika masomo yao na stadi za kazi kwa ujumla ili waweze kufikia malengo yao ya baadae.

Naye Mwakilishi kutoka Shirika la Abbot fund Edna Hauli ameipongeza Serikali kwa juhudi zake katika kuhakiksha watoto wanakuwa salama na kuahidi  kuwa shirika hilo litaendelea kushirikiana na Serikali ili kuhakikisha watoto wanapata mahitaji yao muhimu  na kuweza kufikia utimilifu wao kama binadamu.

Sanjari na hilo katika tukio hilo pia kuliambatana na tukio la kukabidhi mashine ya kufulia 4, printer na photocopy mashine 1, vitabu 1670 friji 2 nguo na mahitaji mengine ambavyo vilitolewa na Shirika la Abbot Fund vikiwa na thamani ya shiling Milioni 88 ili viweze kurahisisha majukumu ya utendaji kazi ndani ya Makao hayo.
 
MWISHO
Share:

TANESCO kuifanya SGR kuwa mkoa wa KI-TANESCO

Published from Blogger Prime Android App


Published from Blogger Prime Android App


Published from Blogger Prime Android App



NA MWANDISHI WETU,DODOMA

URUGENZI Mkuu wa Shirika la Umeme nchini (TANESCO) Mhandisi Gissima Nyamo-Hanga amesema Shirika hilo lipo mbioni kuanzisha mkoa wa ki-TANESCO wa njia ya treni ya umeme (SGR)  ambao utakuwa na kazi moja tu ya kushughulikia njia ya treni hiyo ili kuondoa changamoto za kuzimika njiani.

Mhandisi Nyamo-Hanga ametoa kauli hiyo leo Machi 26 mwaka huu jijini Dodoma wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio ya Shirika hilo katika kipindi Cha miaka minne ya Serikali ya awamu ya sita.

Amesema hatua hiyo ni kufuatia changamoto zilizojitokeza awali za kukatika kwa umeme katika treni hiyo kipindi Cha awali treni hiyo  ilipoanza safari zake.

"Changamoto zilizojitokeza awali kwenye treni ya SGR kuzimika njiani , ni kwa sababu tulikuwa ndio tumeanza uendeshaji wake  na hivyo walikuwa na hatua nyingi za kujifunza kwa TANESCO  na hata kwa upande  wa SGR,kitu kinapokuwa kipya yumkini kinaweza kuleta shida kwa sababu ya ugeni wake ."amesema Mhandisi huyo

Hata hivyo amesema laini ya umeme ya SGR sasa ipo madhubuti na huduma  ya usafiri wa treni inaendelea vizuri .

"Kama shirika ,tutahakikisha SGR tunaichukulia kama mkoa ,kwamba tunaweka menejimenti na Utawala maalum kwa ajili ya mkoa huo..,katika level za kitanesco,katika kila mkoa huwa tuna Meneja wa mkoa ambaye anakuwa na timu ya watu wengi kuanzia ' registration', mafundi,mpaka wahandisi kwa ajili ya kuangalia huduma ya umeme katika mkoa huo."alisema na kuongeza kuwa 

"Timu hiyo itakuwa na kazi ya kushughulika na SGR tu lengo ni kuhakikisha kwamba umeme katika uendeshaji wa treni unakuwa wa uhakika na imara"


Share:

JK AWASILISHA UJUMBE MAALUMU KWA RAIS WA SENEGAL KUTOKA KWA RAIS SAMIA


Published from Blogger Prime Android App



Na Mwandishi wetu

RAIS Mstaafu  Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete amewasilisha  ujumbe maalumu kutoka kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwenda kwa Rais wa Jamhuri ya Senegal, Mhe. Bassirou Diomaye Faye jijini Dakar.

Katika mazungumzo  yao ya kirafiki,  Rais Mstaafu alieleza dhamira ya dhati ya Rais Samia na Serikali anayoiongoza ya kuendeleza na kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia, kiuchumi na kijamii kati ya Tanzania na Senegal.

Pamoja na masuala ya ushirikiano wa kiserikali, Rais Mstaafu pia alisisitiza umuhimu wa kukuza uhusiano baina ya wananchi wa mataifa haya mawili kupitia sekta za elimu, biashara, utalii, na maendeleo ya vijana na wanawake.

Ziara hii ni sehemu ya juhudi endelevu za Tanzania kuimarisha uhusiano wa kimataifa na mataifa ya Afrika Magharibi, huku ikiweka msisitizo kwa diplomasia ya uchumi na ushirikiano wa watu kwa watu.
Share:

Wizara ya Nishati yataja vipaumbele vya bajeti yake mwaka wa fedha 2025/2026

Published from Blogger Prime Android App


Published from Blogger Prime Android App


Published from Blogger Prime Android App



*📌 Rukwa, Kagera, Lindi. Mtwara kuunganishwa na gridi ya Taifa.*

*📌 Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia kuendelea kuhamasishwa*

*📌 Serikali kuendelea kuimarisha utendaji wa Taasisi, Mashirika  chini ya Wizara ya Nishati,*

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ametaja  vipaumbele vya Wizara  ya Nishati katika Bajeti ya mwaka wa fedha 2025/2026 ikiwemo kuendelea kutekeleza miradi ya uzalishaji, usafirishaji,  usambazaji  umeme na kufikisha gridi ya Taifa katika Mikoa iliyosalia ya Rukwa, Kagera, Lindi na Mtwara;

Akiwasilisha vipaumbele hivyo kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Njshati na Madini, leo jijini Dodoma, Dkt. Biteko amesema  vipaumbele hivyo vimezingatia mpango wa Taifa wa Nishati wa mwaka 2025 hadi 2030.

“Mhe. Mwenyekiti vipaumbele hivi vimezingatia mpango wa Taifa wa Nishati wa mwaka 2025 - 2030 (National Energy Compact 2025 - 2030) utakaosaidia upatikanaji na uunganishaji wa umeme kwa wananchi, kuongeza mchango wa nishati jadidifu katika uzalishaji wa umeme na ushiriki wa Sekta Binafsi katika maendeleo ya Sekta ya Nishati ”. Amesema Dkt. Biteko

Katika hatua nyingine, Dkt. Biteko amesema Serikali imewajengea wazawa uwezo mkubwa wa kutekeleza miradi ya umeme huku akitolea mfano wa ajira kwenye miradi ya umeme kufikia idadi ya  53,000.

Amesema  Dunia inahitaji nishati na mahitaji ya umeme yamekuwa yakiongezeka kwa kasi hivyo Serikali itaendelea kuongeza vyanzo vya kuzalisha umeme ili kukidhi mahitaji ya Watanzania.

Awali, Mkurugenzi wa Sera na Mipango, Wizara ya Nishati, Petro Lyatuu alisema kuwa katika kuhakikisha kunakuwa na upatikanaji wa umeme wa uhakika Wizara itaendelea kuimarisha Gridi ya Taifa (National Grid Stabilization Project) pamoja na kufanya matengenezo na ukarabati wa mitambo ya kuzalisha umeme;

“Mhe. Mwenyekiti tutandelea na usambazaji wa nishati katika Vitongoji, maeneo ya migodi, kilimo, viwanda na pampu za maji pamoja na vituo vya afya ili kuwezesha shughuli za
uzalishaji na utoaji wa huduma bora kwa wananchi.” Aliongeza Lyatuu

Kuhusu Nishati Safi ya Kupikia Lyatuu alisema Serikali itaendelea kuhamasisha na kuwezesha watanzania kutumia nishati safi ya kupikia ikiwa ni utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia (2024-2034) na mpango wa Taifa ya Nishati wa mwaka 2025 - 2030 (National Energy Compact 2025 - 2030).

Aliongeza  kuwa Serikali itaendelea na shughuli za utafutaji, uendelezaji na usambazaji wa mafuta na gesi asilia pamoja na kutekeleza miradi ya kielelezo na kimkakati ya mafuta na gesi asilia
ikiwemo Mnazi Bay Kaskazini, Eyasi - Wembere, pamoja na mradi wa Kuchakata na Kusindika Gesi asilia kuwa Kimiminika (Liquefied Natural Gas - LNG Project).

Mradi mwingine ni ujenzi wa Bomba la kusafirisha mafuta ghafi kutoka Hoima, Uganda hadi Tanga, Tanzania (East African Crude Oil Pipeline - EACOP).

Vile vile, amesisitiza kuwa Serikali itaendela kuimarisha utendaji wa Taasisi na Mashirika yaliyo chini ya Wizara ya TANESCO, REA, TPDC, PBPA, EWURA na PURA pamoja na Kampuni Tanzu ili yatoe huduma bora kwa wadau, kuimarisha mapato pamoja na tija na ufanisi katika uendeshaji;

Amesema lengo lingine ni kuongeza  kiwango cha upatikanaji wa umeme kutoka cha sasa cha asilimia 78.4 hadi kufikia asilimia 100 ifikapo mwaka 2030.

Naye, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini, Mhe. David Mathayo ameipongeza Serikali kwa kuja na vipaumbele vitakavyowawezesha watanzania kuwa na nishati ya uhakika.
Share:

TBS lateketwza bidhaa zisizokidhi viwango za sh.bilioni 1.5


Published from Blogger Prime Android App


Joyce Kasiki,Dodoma

SHIRIKA  la Viwango Tanzania (TBS) limeteketeza bidhaa mbalimbali zisizokidhi viwango ya ubora  vyenye thamani ya Shilingi bilioni 1.5 kati ya Julai na Disemba 2024, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kulinda afya na usalama wa watumiaji pamoja na kuzuia uingizaji wa bidhaa hafifu nchini.

Hayo yamesemwa Jana jijini Dodoma na Mkurugenzi  Mkuu wa TBS, Dkt. Ashura Katunzi,wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu utekelezaji wa majukumu ya Taasisi hiyo hasa katika kipindi Cha miaka minne ya Uongozi wa Serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan.

Dkt.Katunzi alisema  kuwa, bidhaa hizo ziliteketezwa baada ya kukutwa na kasoro mbalimbali, zikiwemo kutokuwa na viwango vya ubora vinavyotakiwa, kuwa na viambato hatarishi kwa afya, ama kuingizwa nchini bila kufuata taratibu za kisheria.

“Katika kipindi cha miezi sita, tumeteketeza bidhaa zenye thamani ya Shilingi bilioni 1.5, ikiwa ni hatua madhubuti ya kuzuia bidhaa zisizofaa kufika kwa watumiaji,hii ni sehemu ya mkakati wa TBS wa kuhakikisha soko la Tanzania linakuwa na bidhaa salama na bora kwa wananchi,” alisema Dkt. Katunzi.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi huyo,  bidhaa zilizoteketezwa ni pamoja na vipodozi vyenye viambato vilivyopigwa marufuku, chakula kilichoisha muda wake, vifaa vya umeme visivyokidhi viwango, pamoja na bidhaa nyingine zisizo na usajili wa ubora kutoka TBS.

Alisema, shirika hilo limeendelea kuimarisha mifumo yake ya ukaguzi wa bidhaa zinazoingia nchini, ikiwa ni pamoja na kutumia teknolojia za kisasa katika maabara zake 12 ambazo zote zimepata ithibati ya kimataifa. 

Dkt. Katunzi aliongeza kuwa hatua hii imewezesha kubaini kwa haraka bidhaa hafifu na kuzuia zisifike kwa watumiaji.

Mbali na ukaguzi wa bidhaa zinazoingizwa nchini,  pia TBS imeendelea kutoa mafunzo kwa wazalishaji wa ndani ili kuhakikisha wanazalisha bidhaa zenye ubora unaokidhi viwango vya kitaifa na kimataifa.

 Katika kipindi cha miaka minne iliyopita, shirika hilo limeandaa viwango 1,823 vya sekta mbalimbali na kutoa vyeti na leseni za ubora 2,402 kwa wazalishaji, wakiwemo wajasiriamali wadogo 1,066.

Aidha, TBS imekuwa ikishirikiana na taasisi mbalimbali, vyuo vikuu, na mashirika ya kimataifa ili kuhakikisha mifumo yake ya udhibiti ubora inazidi kuwa na ufanisi mkubwa.

Kwa upande wa wananchi, Dkt. Katunzi aliwataka kuwa makini wanaponunua bidhaa kwa kuhakikisha zinakuwa na alama ya ubora ya TBS na kuepuka bidhaa zisizo na usajili wa shirika hilo. Pia alihimiza wananchi kutoa taarifa kwa mamlaka husika pindi wanapobaini bidhaa zisizokidhi viwango zikiuzwa sokoni.

Alisema, TBS   litazidi kuchukua hatua kali dhidi ya wahusika wanaoingiza au kusambaza bidhaa hafifu nchini, ikiwa ni pamoja na kutaifisha na kuteketeza bidhaa hizo, pamoja na kuwachukulia hatua za kisheria wahusika wote.


Share:

TANZANIA, BARBADOS KUIMARISHA USHIRIKIANO


Published from Blogger Prime Android App



📌 Dkt. Biteko afanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Barbados

📌 Wakubaliana kuwekeza katika Ushirikiano Sekta ya Utalii na Maji 

📌 Nishati Safi ya Kupikia, M300 kivutio cha mazungumzo
 
Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Barbados, Mhe. Mia Mottley ambapo wamekubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo mbili.

Mazungumzo hayo yamefanyika  katika makazi rasmi ya Waziri Mkuu, Mhe. Mia Mottley, Jijini Bridgestone, nchini Barbados.

Waziri Mkuu Mia amesema, kuna umuhimu wa kuwa na mkakati wa pamoja na kushirikiana kwa lengo la kukuza utalii kati ya Barbados na Tanzania na nchi za Afrika Mashariki kwa ujumla. Amesema kuna maeneo mengi ya vivutio vya utalii ambavyo vinaweza kuzinufaisha pande hizo mbili yakiwemo masuala ya ukarimu.

Maeneo mengine ya ushirikiano ni katika utoaji wa mafunzo maeneo ya ufundi kati ya nchi za Carib (Caribbean) na nchi mbalimbali za kiafrika huku akisisitiza kuwa umuhimu wa uboreshaji wa masoko na kubadilishana wataalam katika sekta mbalimbali kwa makubaliano maalum.

Aidha, amesema upo uhitaji wa wataalam katika sekta ya maji na miundombinu na hivyo kuna uwezekano wa kubadilishana wataalam ili kujengeana uzoefu katika sekta mbalimbali kulingana na makubaliano yatakayofikiwa.

Kwa upande wake, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Biteko amesema mapendekezo hayo ni mazuri na yanaweza kuwa matokeo chanya baada ya kuchambuliwa na watalaam katika sekta husika kupitia Wizara zinazohusika na masuala ya kidiplomasia.

Dkt. Biteko amesema Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa Rais, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendeleza kampeni ya Nishati Safi ya Kupikia ambayo inalenga kuwawezesha asilimia 80 ya watumiaji wa nishati kuondokana na matumizi ya nishati isiyokuwa safi ifikapo mwaka 2034.

Katika utekelezaji wa mpango huo, amesema Tanzania inatembea kifua mbele kunadi mkakati huo wa miaka 10 ambao pamoja na mambo mengine unakusudia kupunguza madhara kwa watumiaji wa nishati isiyokuwa safi inayopelekea uchafuzi wa mazingira, magonjwa ya kupumua pamoja na vifo.

“Januari mwaka huu tumekuwa na mkutano wa Wakuu wa nchi za Afrika (M300) uliofanyika jijini Dar es Salaam ukilenga kuwa wezesha watu milioni 300 barani Afrika ambao hawajaona umeme kuweza kupata haki hiyo ikiwa ni miaka mitano kuanzia sasa na baada ya hapo itaweka namna tunavyoweza kusonga mbele kulingana na matokeo yanayofikiwa” amesema Dkt. Biteko.

Dkt. Biteko amefafanua kuwa, hatua ya Tanzania kushiriki katika mkutano wa nishati endelevu kwa wote (SEforALL) uliofanyika nchini Barbados, ni kuthibitisha nia yake thabiti inayolenga matokeo chanya. Hivyo, amesema yapo maeneo mengi ya kushirikiana na kuwezesha wananchi wa pande zote mbili kupata maendeleo na ustawi wa pamoja.

Mkutano wa Dkt. Biteko Waziri Mkuu wa Barbados, umehitimisha ziara ya kikazi nchini humo ambako alishiriki katika Kongamano la kimataifa la nishati endelevu kwa wote pamoja na mikutano ya wadau mbalimbali iliyojikita katika uboreshaji wa sekta ya nishati kwa manufaa ya nchi hizo mbili. 

Katika ziara hiyo, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, alifuatana na Waziri wa Maji, Nishati na Mhe. Shaib Kaduara, Balozi wa Tanzania nchini Cuba, Mhe. Humphrey Polepole, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mha. Felichesmi Mramba na Mshauri wa Rais katika masuala ya Nishati na Maendeleo ya Jamii, Mhe. Angellah Kairuki.

Mwisho.
Share:

NAIBU WAZIRI MWANAIDI APONGEZA KAMATI YA MTAKUWWA KARATU



Published from Blogger Prime Android App


Na WMJJWM - Karatu- Arusha

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mwananidi Ali Khamis, ameridhishwa na Maendeleo ya utekelezaji wa Mpango Kazi wa Kwanza wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (2017/18 – 2021/22)

Amesema hayo Machi 14, 2025 akiwa katika ziara Wilaya ya Karatu  kwa lengo la ufuatiliaji na tathimini ya utekelezaji wa programu za malezi mbadala pamoja na programu ya uwezeshaji wa uchumi wa familia na vijana zinazotekelezwa na Shirika la SOS katika Mkoa wa Arusha.

Naibu Waziri Mwananidi amepongeza Kamati za MTAKUWWA katika ngazi zote kwa kuendelea kuwa waadilifu katika kusimamia na kutekeleza majukumu yenu kikamilifu na kuimarisha ulinzi wa mwanamke na mtoto.

"Endeleeni kuzingatia matakwa ya Mwongozo wa MTAKUWWA na kuanzisha kamati katika ngazi ya Wilaya, Kata na Mitaa kwa lengo la kupunguza aina zote za vitendo vya ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto" amesema Naibu Waziri Mwananidi.

Ameongeza kwamba Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum kwa kushirikiana Wizara za Kisekta inatekeleza Mpango Kazi wa Pili wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA II 2024/25 hadi 2028/29 kwa lengo kupunguza aina zote za ukatili kwa asilimia 50.

Akiyataja mafanikio ya utekelezaji wa  Mpango Kazi wa Kwanza wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili Dhidi ya Wanawake na Watoto (2017/18 – 2021/22) amesema Mpango huo umesaidia kuongezeka kwa huduma za mikopo yenye masharti nafuu kupitia mifuko tofauti. Mfano mikopo ya asilimia10 inayotokana na ya mapato ya ndani ya Halmashauri kutoka Shilingi Bilioni 15.6 mwaka 2017/28 hadi Shilingi Bilioni 35.6 mwaka 2021/22.

Mafanikio mengine ni kupungua kwa vitendo vya ukatili wa  kingono kwa Wanawake kutoka asilimia 17 mwaka 2015 hadi asilimia 12 mwaka 2022, pamoja na kuongezeka kwa Vituo vya kulelea Watoto Wadogo mchana (ECD Centers)  kutoka 1,103 hadi 2,649.

Aidha, Naibu Waziri Mwananidi amelipongeza Shirika la SOS kwa kuendelea kushirikiana na Serikali kuimarisha kamati za MTAKUWWA kuanzia ngazi ya Wilaya hadi Vijjijini pamoja na kuwaomba viongozi wa Kamati hizo kutatua changamoto zinazowakabili ikiwa ni pamoja na kuwajengea uwezo kwa kuwapatia mafunzo stahiki ili waweze kutimiza majukumu yao kwa ufanisi mzuri zaidi.


Share:

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Labels

Blog Archive

Recent Posts

Unordered List

  • Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  • Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  • Vestibulum auctor dapibus neque.

Pages

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.