RAIS DKT. SAMIA AZUNGUMZA WAKATI WA KULIFUNGA BUNGE LA 12: "WABUNGE MMETIMIZA WAJIBU WENU KWA WELEDI NA UZALENDO"


Published from Blogger Prime Android App



Na Joyce Kasiki,DODOMA

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amelihutubia Bunge la Kumi na Mbili katika hafla ya kulifunga rasmi, huku akilipongeza Bunge hilo kwa kazi kubwa na nzuri ya kutunga sheria, kuisimamia serikali, na kuwakilisha wananchi kwa weledi na uzalendo mkubwa.

Akizungumza ndani ya Ukumbi wa Bunge jijini Dodoma, Rais Samia alimpongeza Mheshimiwa Spika Dkt. Tulia Ackson kwa kuliongoza Bunge kwa umahiri mkubwa, licha ya changamoto zinazotokana na tofauti za kisiasa na mitazamo ya wabunge mbalimbali.

"Mheshimiwa Spika, kuliongoza Bunge si kazi rahisi. Kwenye wengi kunamengi, lakini kwa umahiri wako na weledi, umeweza kuivusha mashua yetu salama hadi bandari, kama manahodha mahiri wa baharini,” alisema Rais Samia huku akishangiliwa na wabunge.

Rais Samia pia alitambua mafanikio ya kihistoria ya Spika Dkt. Tulia Ackson kwa kuwa mwanamke wa kwanza barani Afrika kushika nafasi ya Urais wa Mabunge ya Afrika (PAP), akisema mafanikio hayo yameongeza heshima ya Tanzania kimataifa.

Katika hotuba yake, Rais aliwapongeza wabunge wote kwa kutekeleza majukumu yao kikamilifu na kushiriki kikamilifu katika kujadili sera na mipango ya maendeleo ya taifa. Alisema kuwa Bunge hilo limekuwa na mchango mkubwa katika kujenga ustawi wa wananchi na kuleta maendeleo ya kweli.

"Nitumie fursa hii kulitushukuru Bunge kwa tuzo mlionipatia. Ninathamini kwa dhati kutambua kwenu mchango wangu katika maendeleo na ustawi wa nchi yetu,” alisema Rais.

Share:

No comments:

Post a Comment

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Labels

Recent Posts

Unordered List

  • Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  • Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  • Vestibulum auctor dapibus neque.

Pages

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.