
Na Joyce Kasiki,DODOMA
RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, amelitaka Jeshi la PolisiNchini kkuongeza nguvu katika kukomesha matukio ya watu kupotea nchini.
Rais Dkt.Samia ameyasema hayo Bungeni Jijini Dodoma , Leo Juni 27,2025 wakati akihitimisha rasmi Bunge la 12
Amesema kuwa pamoja na mafanikio makubwa yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitano ya Bunge hilo, bado yapo mambo yanayohitaji kushughulikiwa kwa dharura, likiwemo suala la usalama wa raia, hasa katika matukio ya watu kutoweka bila maelezo.
"Jeshi la Polisi lina wajibu wa kuhakikisha usalama wa wananchi, na mojawapo ya vipaumbele vyake sasa ni kuhakikisha kuwa matukio ya watu kupotea yanakomeshwa kabisa,” alisisitiza Rais Dkt. Samia
No comments:
Post a Comment