Rais Dkt.Samia kuchukua fomu kesho kuwania urais




Published from Blogger Prime Android App


Na Mwandishi wetu Dodoma 

MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa, ambaye pia ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuchukua fomu ya kugombea nafasi ya Urais kwa tiketi ya CCM, tarehe 9 Agosti 2025, katika Ofisi za Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC).

Zoezi hilo linaashiria kuanza rasmi kwa mchakato wa kampeni za uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, unaotarajiwa kufanyika tarehe 29 Oktoba mwaka huu, kwa vyama vyote vya siasa nchini.

Akizungumza leo, Agosti 8, jijini Dodoma, Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM, CPA Amos Makalla, amethibitisha kuwa chama hicho kipo tayari kikamilifu kwa hatua hiyo muhimu ya kidemokrasia. Aidha, alieleza kuwa baada ya kuchukua fomu hiyo, Dkt. Samia atapokelewa katika Ofisi za Makao Makuu ya CCM, Dodoma, ambako atapata nafasi ya kusalimiana na wananchi.

CPA Makalla amesisitiza kuwa kwa kuwa mgombea Urais anatokana na Chama Cha Mapinduzi, hatua hiyo ni sehemu ya mchakato wa utekelezaji wa maamuzi ya vikao vya juu vya chama kuhusu kuwania nafasi ya Urais kwa kipindi kijacho.

Ikumbukwe kuwa Dkt. Samia Suluhu Hassan anachukua fomu hiyo kuwania nafasi ya Urais kwa muhula wa pili wa miaka mitano, ikiwa ni sehemu ya kukamilisha safari ya uongozi wake aliyoianza mwaka 2021.
Share:

No comments:

Post a Comment

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Labels

Recent Posts

Unordered List

  • Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  • Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  • Vestibulum auctor dapibus neque.

Pages

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.