SOS Children's Village yakabidhi Mwongozo wa Taifa wa Uanzishaji, Uendeshaji na Usimamizi wa makao ya watoto


Published from Blogger Prime Android App



Na WMJJWM- Dodoma 

KATIBU  Mkuu wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu amepokea ugeni kutoka  Shirika la Watoto la SOS Children's Village  ambapo ugeni huo ukiongozwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika hilo  Aisha Salim Ali leo Machi 27, 2025 katika Ofisi za Wizara jijini Dodoma.

Dkt Jingu amelipongeza Shirika hilo kwa jitihada zake za kushirikiana na Serikali katika kuhakikisha  wanadhibiti changamoto ya watoto kuishi na kufanya kazi mitaani baada ya Shirika hilo kukabidhi Mwongozo wa Taifa wa Uanzishaji, Uendeshaji na Usimamizi wa makao ya watoto nchini.

Aidha Dkt. Jingu ametoa wito kwa jamii kuimarisha taasisi ya familia na kuepuka migogoro kwani tafiti zinaonesha hivi karibuni kumekua na kuvunjika kwa ndoa nyingi  na  kupelekea kupatikana kwa wimbi la watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la SOS Children's Village   Aisha Salim Ali ameahidi ushirikiano kati ya Shirika lake na Wizara katika kuhudumia Watoto katika Makao ya Watoto kwa kuweka namna nzuri ya Utoaji wa huduma na Malezi katika Makao hayo.

Mwisho.
Share:

Related Posts:

No comments:

Post a Comment

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Labels

Unordered List

  • Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  • Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  • Vestibulum auctor dapibus neque.

Pages

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.