Serikali yaombwa kupeleka maji Tukuyu Kutoka Ziwa Nyasa




Published from Blogger Prime Android App



DODOMA

MBUNGE wa Viti Maalum Sophia Mwakagenda ameiomba Serikali kupeleka maji Mji wa Tukuyu Kutoka Ziwa Nyasa Ili kusaidia wananchi wa wilaya hiyo kupata maji safi na salama.

Akiuliza swali la nyongeza Bungeni jijini Dodoma Mwakagenda amesema  Mji wa Tukuyu hauna maji huku alihoji lini Serikali itapeleka fedha ili kujenga mradi wa kutoa maji Ziwa Nyasa na kuyafikisha Mji wa Tukuyu.

"Kama ilivyo kwa ziwa Victoria, tuna Ziwa Nyasa na Mji wa Tukuyu hauna maji, ni lini Serikali italeta fedha kuhakikisha maji yanatoka Ziwa Nyasa Hadi kufika  Tukuyu?

Akijibu swali hilo Waziri wa Maji Jumaa Aweso amesema Moja ya mikakati iliyopo Serikalini ni kuhakikisha rasilimali zilizopo nchini zinatumika na kutatua changamoto za wananchi.

"Nimhakikishie Mheshimiwa  Mbunge kwamba Moja ya mikakati na maelekezo ni kuhakikisha rasilimali zilizopo nchini zinatumika na kutatua matatizo ya maji,kwa  hiyo maeneo ya Ziwa Nyasa ni moja ya mikakati ya Wizara ,na Wizara ipo katika hatua mbalimbali kufanya 'visibility Study' ,naamini wananchi wa maeneo hayo pia watanufaika kupata Huduma ya maji safi na salama."amesisitiza Aweso
Share:

Related Posts:

No comments:

Post a Comment

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Labels

Unordered List

  • Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  • Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  • Vestibulum auctor dapibus neque.

Pages

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.