Kapinga amtilia shaka MF Contractor






Published from Blogger Prime Android App



Na Joyce Kasiki,DODOMA


NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amemuelekeza Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kukutana na Mkandarasi MF anayetekeleza mradi wa umeme katika vijiji 15 vya Wilaya ya Nyasa, ili kuangalia uwezekano wa kuteua wakandarasi wadogo (sub-contractors) kutokana na udhaifu wa mkandarasi huyo katika utekelezaji wa kazi.

Kapinga alitoa maelekezo hayo kufuatia swali la nyongeza lililoulizwa Bungeni jijini Dodoma Aprili 24,2025 na Mbunge wa Nyasa, Mhandisi Stella Manyanya, ambaye alitaka wakandarasi waondolewe kutokana na kutokuwepo kwa maendeleo yoyote ya kazi katika maeneo husika.

"Pamoja na pongezi kwa Wizara ya Nishati, lakini kwa kuwa vitongoji vyote vilivyopangiwa kupata umeme awamu hii kupitia wakandarasi MF na Triple C (CCC), hakuna hata kimoja kilichowashiwa umeme. Kwa nini wasiondolewe na kuwekwa wakandarasi wenye uwezo?" alihoji Manyanya.

Akijibu hoja hiyo, Naibu Waziri Kapinga alifafanua kuwa mkandarasi anayetekeleza mradi wa vitongoji hivyo ni kampuni ya CCC na alimtaja kuwa ni mkandarasi mzuri, ambaye kwa sasa yupo katika hatua za manunuzi na atatembelea eneo la mradi hivi karibuni.

Hata hivyo, kuhusu Mkandarasi MF, Kapinga alisema:
"Namuelekeza Mkurugenzi Mkuu wa REA, na tayari tulishazungumza, afanye utaratibu wa kukutana naye ili watafute 'sub-contractors' kwa sababu uwezo wake tayari unatia mashaka. Tutasimamia hili kwa karibu ili kuhakikisha kuwa mradi unakamilika kwa wakati." alisisitiza Kapinga.



Share:

Related Posts:

No comments:

Post a Comment

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Labels

Unordered List

  • Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  • Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  • Vestibulum auctor dapibus neque.

Pages

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.