DktJafo aeleza mafanikio makubwa kiuchumi kupitia sekta ya viwanda

 





Na Mwandishi wetu,Dodoma


WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jafo, amewasilisha hotuba ya bajeti ya wizara yake kwa mwaka wa fedha 2025/2026 mbele ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambapo ametaja mafanikio makubwa na mikakati kabambe inayolenga kukuza uchumi wa viwanda na biashara nchini.

 

Aidha hotuba ya Waziri Jafo imeonesha mwelekeo chanya wa ukuaji wa sekta ya viwanda na biashara nchini ambapo kupitia bajeti aliyoiwasilisha amesema, serikali inaendelea kujenga msingi wa uchumi wa viwanda unaoendeshwa na ubunifu, ushindani, na uendelevu wa masoko ya ndani na nje.


Akisoma hotuba hiyo Bungeni jijini Dodoma, Dkt. Jafo ameliomba Bunge kuidhinisha jumla ya shilingi 135.8 bilioni kwa ajili ya kutekeleza majukumu ya wizara ambapo kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 93.9 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida huku shilingi bilioni 41.9 zikitengwa kwa ajili ya matumizi ya maendeleo.

 

Amesema kuwa  sehemu kubwa ya matumizi ya kawaida ni mishahara ya wafanyakazi, inayofikia shilingi bilioni 75.8, huku bilioni 18.1 zikitengwa kwa matumizi mengineyo.

 

Jafo ametaja vipaumbele vya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha wa 2025/2026 kuwa ni pamoja na  kuendeleza Viwanda, Masoko, na Maendeleo ya Watu.

 

Kwa mujibu wa waziri huyo , katika mwaka ujao, wizara yake imepanga kuendeleza juhudi za kuimarisha sekta ya viwanda kwa kuwezesha uanzishwaji wa viwanda vipya, kuendeleza viwanda vya kimkakati, na kujenga miundombinu ya viwanda vidogo na vya kati (industrial clusters).

 

Aidha, amesema kuwa wizara itaendelea kuboresha mazingira ya biashara na kuvutia uwekezaji, kuimarisha upatikanaji wa masoko ya bidhaa za Tanzania ndani na nje ya nchi, pamoja na kusimamia ubora na usalama wa bidhaa ikiwemo chakula na vipodozi.

 

Kuhusu  uwanja wa biashara, wizara imepanga kuendeleza jitihada za kufungua masoko mapya, kurasimisha biashara mipakani, na kufanya utafutaji wa masoko  ili kusaidia wafanyabiashara kufikia fursa zinazojitokeza.

 

Mauzo ya Bidhaa yavunja rekodi

 

Dkt.Jafo amesema,katika miaka minne iliyopita, Tanzania imepiga hatua kubwa katika mauzo ya bidhaa nje ya nchi ambapo alisema,

Mauzo katika soko la SADC yaliongezeka kwa asilimia 127.7, kutoka dola milioni 1,303.4 mwaka 2021 hadi dola milioni 2,968 mwaka 2024.

 

Katika soko la Afrika Mashariki (EAC) amesema, mauzo yalipanda kutoka dola milioni 1,161.2 hadi 1,163.8 mwaka 2024 huku jumla ya mauzo katika bara la Afrika yamefikia dola milioni 3,946.76 mwaka 2024, ikiwa ni ongezeko la asilimia 61.2 tangu mwaka 2021.

 

Ametaja bidhaa zilizochangia ongezeko hilo ni pamoja na madini, pamba, kahawa, parachichi, saruji, sabuni, na bidhaa za kilimo.

 

AfCFTA: Tanzania yapanua wigo wa Biashara Afrika

 

Kwa mujibu wa Waziri Jafo, Tanzania imekuwa miongoni mwa nchi zinazofaidika na Soko la Biashara Huru la Afrika (AfCFTA), ambapo hadi Machi 2025 nchi imefanikiwa kusafirisha bidhaa kwenda mataifa 18 ya Afrika kwa kutumia vyeti vya uasili wa bidhaa. Bidhaa hizo ni pamoja na nyuzi za mkonge, vioo, kahawa na mchele.

 

Soko la Kimataifa: Marekani na Umoja wa Ulaya

 

Waziri Jafo pia alieleza mafanikio ya Tanzania katika soko la Marekani kupitia mpango wa AGOA, ambapo mauzo yameongezeka kutoka dola milioni 33.06 mwaka 2021 hadi dola milioni 85.4 mwaka 2023 – sawa na ongezeko la asilimia 158.3. Bidhaa maarufu zilizouzwa ni nguo, kahawa na mbogamboga.

 

Kwa upande wa Umoja wa Ulaya (EU), mauzo yameongezeka kwa asilimia 38.5, kutoka dola milioni 891.5 mwaka 2021 hadi dola milioni 1,234.3 mwaka 2024. Bidhaa zilizouzwa ni pamoja na mazao ya chakula, madini, maua, na ngozi.

 

Vikwazo vya Biashara: Serikali Yashughulikia Changamoto

 

Katika juhudi za kuvutia biashara zaidi, serikali imefanikiwa kutatua jumla ya vikwazo vya kibiashara 70 kati ya Tanzania na nchi jirani, vikiwemo Kenya na Zambia. 


Kwa mujibu wa Waziri Jafo,hatua hiyo imesaidia kurahisisha biashara mipakani na kuongeza ushirikiano wa kiuchumi kikanda.

 


Share:

Kapinga amtilia shaka MF Contractor






Published from Blogger Prime Android App



Na Joyce Kasiki,DODOMA


NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amemuelekeza Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) kukutana na Mkandarasi MF anayetekeleza mradi wa umeme katika vijiji 15 vya Wilaya ya Nyasa, ili kuangalia uwezekano wa kuteua wakandarasi wadogo (sub-contractors) kutokana na udhaifu wa mkandarasi huyo katika utekelezaji wa kazi.

Kapinga alitoa maelekezo hayo kufuatia swali la nyongeza lililoulizwa Bungeni jijini Dodoma Aprili 24,2025 na Mbunge wa Nyasa, Mhandisi Stella Manyanya, ambaye alitaka wakandarasi waondolewe kutokana na kutokuwepo kwa maendeleo yoyote ya kazi katika maeneo husika.

"Pamoja na pongezi kwa Wizara ya Nishati, lakini kwa kuwa vitongoji vyote vilivyopangiwa kupata umeme awamu hii kupitia wakandarasi MF na Triple C (CCC), hakuna hata kimoja kilichowashiwa umeme. Kwa nini wasiondolewe na kuwekwa wakandarasi wenye uwezo?" alihoji Manyanya.

Akijibu hoja hiyo, Naibu Waziri Kapinga alifafanua kuwa mkandarasi anayetekeleza mradi wa vitongoji hivyo ni kampuni ya CCC na alimtaja kuwa ni mkandarasi mzuri, ambaye kwa sasa yupo katika hatua za manunuzi na atatembelea eneo la mradi hivi karibuni.

Hata hivyo, kuhusu Mkandarasi MF, Kapinga alisema:
"Namuelekeza Mkurugenzi Mkuu wa REA, na tayari tulishazungumza, afanye utaratibu wa kukutana naye ili watafute 'sub-contractors' kwa sababu uwezo wake tayari unatia mashaka. Tutasimamia hili kwa karibu ili kuhakikisha kuwa mradi unakamilika kwa wakati." alisisitiza Kapinga.



Share:

Serikali yaombwa kupeleka maji Tukuyu Kutoka Ziwa Nyasa




Published from Blogger Prime Android App



DODOMA

MBUNGE wa Viti Maalum Sophia Mwakagenda ameiomba Serikali kupeleka maji Mji wa Tukuyu Kutoka Ziwa Nyasa Ili kusaidia wananchi wa wilaya hiyo kupata maji safi na salama.

Akiuliza swali la nyongeza Bungeni jijini Dodoma Mwakagenda amesema  Mji wa Tukuyu hauna maji huku alihoji lini Serikali itapeleka fedha ili kujenga mradi wa kutoa maji Ziwa Nyasa na kuyafikisha Mji wa Tukuyu.

"Kama ilivyo kwa ziwa Victoria, tuna Ziwa Nyasa na Mji wa Tukuyu hauna maji, ni lini Serikali italeta fedha kuhakikisha maji yanatoka Ziwa Nyasa Hadi kufika  Tukuyu?

Akijibu swali hilo Waziri wa Maji Jumaa Aweso amesema Moja ya mikakati iliyopo Serikalini ni kuhakikisha rasilimali zilizopo nchini zinatumika na kutatua changamoto za wananchi.

"Nimhakikishie Mheshimiwa  Mbunge kwamba Moja ya mikakati na maelekezo ni kuhakikisha rasilimali zilizopo nchini zinatumika na kutatua matatizo ya maji,kwa  hiyo maeneo ya Ziwa Nyasa ni moja ya mikakati ya Wizara ,na Wizara ipo katika hatua mbalimbali kufanya 'visibility Study' ,naamini wananchi wa maeneo hayo pia watanufaika kupata Huduma ya maji safi na salama."amesisitiza Aweso
Share:

Sekiboko ahoji mkakati wa Serikali kuboresha soko la machungwa Tanga




Published from Blogger Prime Android App



MBUNGE wa Viti Maalum Husna Sekiboko amehoji hatua zinazochukukiwa na Serikali Ili kulinda Kilimo Cha matunda kwa lengo lai kuokoa soko la matunda linalosuasua kutokana na uingizaji mkubwa wa matunda nchini.

Akiuliza swali Bungeni Sekiboko pia amesema "Mkoa wa Tanga ni maarufu kwa Kilimo cha matunda hasa machungwa lakini bado hayajapati soko zuri kwenye viwanda,ni upi mkakatii wa Serikali katika kuboresha Kilimo Cha matunda ili kuweza kukidhi mahitaji ya viwandani?amehoji Sekiboko na kuongeza kuwa 

"Pamekuwa na changamoto kubwa ya kuoza matunda kabla ya kufika sokoni ,ni upi mkakati wa Serikali wa kujenga vyumba baridi kwa ajili ya kuhifadhi matunda ."

Akijibu maswali hayo ,Naibu Waziri wa Kilimo David Silinde amesema katika  kulinda soko na kudhibiti uingiaji holela wa matunda nchini, Serikali imechukua hatua mbalimbali zikiwemo kuanzisha Mamlaka ya Udhibiti wa Nafaka na Mazao Mchanganyiko (COPRA) ambayo itaweka utaratibu wa kuwezesha uingizaji na usafirishaji nje wa mazao ya nafaka na mazao mchanganyiko yakiwemo matunda.

"Pia imeamasisha uanzishaji wa viwanda vya kusindika matunda ili kuimarisha soko la ndani na kupunguza upotevu,kutoa ruzuku ya pembejeo kwa mazao ya matunda ikiwemo maembe, machungwa na parachichi ili kuongeza tija na kuimarisha utafiti na uzalishaji wa mbegu na miche bora ya matunda kulingana na mahitaji ya soko.

 Aidha Silinde amemthibitishia Mbunge huyo kwamba Serikali, inatambua mkoa wa Tanga ni Moja ya Mkoa unaotegemewa  kwa Kilimo cha machungwa .

"Tunakiri kwamba kuna changamoto kubwa ya kuoza kwa matunda hayo ambayo imekuwa ni Moja ya jitihada kubwa zinazofanywa na Serikali kuokoa matunda hayo ambapo kazi kubwa iliyofanyika sasa hivi ni kuhamasisha sekta Binafsi kuingia katika kujenga viwanda vidogo vidogo kwa ajili ya kuongeza thamani ya mazao haya kama vile Kutoka katika tunda kuwa juisi  na Tanga ndio mkoa ambao sasa hivi tumeuweka kwenye mkakati huo."amesema Silinde

Kuhusu kuoza mazao amesema,Serikali inao Mpango madhubuti na tayari  imepata fedha kwa ajili ya kujenga vyumba baridi kwa ajili ya kuhifadhi haya matunda
Share:

Tanzania ilivyojidhatiti maonesho ya Expo 2025 Osaka,Japan






Published from Blogger Prime Android App



Na Joyce Kasiki,DODOMA

WAZIRI  wa Viwanda na Biashara, Dkt. Selemani Jaffo, amesema kuwa Tanzania imejipanga kushiriki kikamilifu katika Maonesho ya Dunia ya EXPO 2025 yatakayofanyika mjini Osaka, Japan kuanzia Aprili 12 hadi Oktoba 13, 2025 kwa lengo la kutangaza fursa za biashara, uwekezaji, utalii, pamoja na Mila na Utamaduni wa Taifa.

Akizungumza leo jijini Dodoma na waandishi wa habari, Dkt. Jaffo amesema EXPO ni maonesho makubwa ya kimataifa yanayoratibiwa na Bureau of International Exposition (BIE) ambapo nchi wanachama, ikiwemo Tanzania, hupiga kura kuchagua mwenyeji wa maonesho hayo.

“TanTrade kwa niaba ya Serikali ya Tanzania, imekuwa ikiratibu ushiriki wa nchi yetu kwenye EXPO tangu mwaka 1967. Hadi sasa tumeshiriki katika EXPO takriban tisa, ikiwemo Expo 2020 Dubai na Expo ’70 Japan. Ushiriki huu umekuwa jukwaa muhimu la kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na kiuchumi,” alisema Waziri Jaffo.

EXPO 2025 Osaka inabeba kauli mbiu kuu isemayo “Kuwezesha jamii kwa Maisha Endelevu” ambapo Tanzania imechagua kaulimbiu ndogo ya “Kuunganisha Maisha – Connecting Lives” yenye malengo ya kuunganisha uzalishaji wa ndani na masoko ya nje, kuhamasisha uwekezaji, kuimarisha mawasiliano ya kiteknolojia, na kuchochea sekta ya utalii.

Dkt. Jaffo amesema Tanzania ni miongoni mwa nchi zaidi ya 160 zilizothibitisha ushiriki wake rasmi, na kwamba banda la Tanzania litakuwa na ukubwa wa mita za mraba 53 kwa ajili ya maonesho na mita za mraba 15 kwa ajili ya biashara.

“Kwa Expo 2025 Osaka, tuna matarajio makubwa zaidi. Tunaamini tutaongeza upatikanaji wa masoko ya bidhaa za Tanzania, kuimarisha uchumi wa nchi, na kuvutia wawekezaji wa kimkakati kupitia ushirikiano na sekta binafsi,” amesema Dkt. Jaffo.

Amesema maonesho hayo pia yataambatana na programu maalum za kila wiki, ikiwemo Utalii, Miundombinu, Kilimo na Uchumi wa Buluu, Afya, Sanaa na Utamaduni, Nishati na Sayansi na Teknolojia. Kila programu itaratibiwa na Wizara husika kwa kushirikiana na taasisi na sekta binafsi.

Aidha, Siku ya Tanzania katika EXPO hiyo imepangwa kufanyika Mei 25, 2025 ambapo mgeni rasmi atakuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa. Siku hiyo itafuatiwa na Kongamano la Biashara, Uwekezaji na Utalii litakalofanyika Mei 26, 2025.

Waziri Jaffo alitoa wito kwa taasisi za umma, mashirika ya kimataifa na binafsi kushiriki kikamilifu katika maandalizi na maonesho hayo kwa kuwasilisha maudhui ya miradi ya kimkakati, kuthibitisha ushiriki katika programu na kongamano, pamoja na kuandaa mapendekezo ya maeneo ya ushirikiano na taasisi za Kijapani.

“Washiriki wote wanatakiwa kujisajili kupitia tovuti ya TANTRADE au kwa kutumia QR code inayotangazwa kupitia vyombo vya habari,” alihitimisha.

EXPO 2025 Osaka ni fursa adhimu kwa Tanzania kuonesha dunia nguvu yake ya kiuchumi, vivutio vyake vya kiutalii, pamoja na uwezo wake mkubwa katika ubunifu, teknolojia na maendeleo ya jamii.
Share:

Rais Samia aitaka Mahakama kutenda haki bila kuangalia hali ya mtu




Published from Blogger Prime Android App


Na Mwandishi wetu, DODOMA 

RAIS Dkt.Samia Suluhu Hassan amewataka watendaji wa Mahakama kuhakikisha kasi ya utoaji haki kwa wananchi inaendana na ubora wa jengo jipya  la Makao Makuu ya Mahakama ya Tanzania ambalo limejengwa kwa maslahi mapana ya wananchi na Taifa kwa ujumla.

Dkt.Samia ametoa kauli hiyo wakati wa hafla ya uzinduzi wa jengo hilo  sambamba na jengo la Utumishi wa Mahakama na Makazi ya Majaji ambayo yote kwa pamoja yamegharimu kiasi Cha shilingi bilioni 185.4.

Amesema kuwa na majengo mazuri ni kwa ajili ya kujenga mazingira mazuri ya utendaji kazi hasa ya utoaji haki kwa wananchi.

Dkt.Samia amesema,mazingira hayo mazuri yaendane na ubora wa huduma zinazotolewa katika majengo hayo .

Amesema ,Serikali imefanya kazi kubwa ya kujenga mazingira mazuri ya utendaji kazi kwa Majaji hapa nchini na kuwataka nao kufanya kazi ya utoaji haki bila kuangalia Hali ya mtu.

Aidha Dkt Samia ameipongeza Mahakama kwa  ujenzi wa jengo hilo  ambalo limezingatia matumizi ya TEHAMA huku akionyesha kufurahishwa na Mifumo ya Mahakama kusomana.

Amesema ,Mifumo hiyo inamwezesha mtu kuangalia mwenendo wa kesi katika mkoa wowote anaoutaka.

Ametumia nafasi hiyo kuhimiza Mahakama kuendelea kuifanya Mifumo yake kusomana Ili kurahisisha kazi ya utoaji haki na kupunguza mrundikano wa kesi mahakamani.

Amesema,kwa upande wa Serikali imeendelea kuongeza bajeti ya Mahakama Kila mwaka Kutoka bilioni 161 Hadi shilingi bilioni 321 mwaka huu wa fedha kwa lengo la kurahisisha utendaji kazi wa Mahakama.

Kwa upande wake Jaji Mkuu wa Tanzania Prof.Ibrahim Hamis Juma ameishukuru Serikali kwa kuiwezesha Mahakama kupata jengo hilo zuri na hivyo Makao Makuu ya Mahakama kuhamia Dodoma.

"Tunashukuru mheshimiwa Rais kwa kuiwezesha Mahakama kufanya maboresho kupitia mipango yake  ,bila uwezeshaji mipango yetu ingebaki kwenye makaratasi."alisema Prof.Ibrahim

Share:

Wizara ya Habari Ndiyo Roho ya Nchi - Mhe. Abdulla



Published from Blogger Prime Android App


Na Adelina Johnbosco - MAELEZO

Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, amesema Wizara ya Habari  ni muhimu sana katika nchi kutokana na majukumu yake ya uhabarishaji wa masuala mbalimbali katika kila nyanja ndani na nje ya Tanzania. 

Amesema hayo leo Aprili 3, 2025 katika Hoteli ya New Amaan Zanzibar wakati akifungua Kikao Kazi cha 20 cha Maafisa Habari wa Serikali kitakachodumu hadi Aprili 6, 2025.

"Wizara ya Habari ina mambo mengi, na ndiyo roho ya nchi, wengine wanasema ni Wizara ya Fedha, lakini hata fedha zenyewe zinataka habari, unaweza kuwa nazo ukazitumia lakini bila ya habari zisionekane matumizi yake" amesisitiza Mhe. Abdulla 

Vile vile, amewashukuru Maafisa Habari kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kutekeleza majukumu yao ya kuuhabarisha umma na ulimwengu kwa ujumla kuhusu mafanikio ya Serikali.

"Kazi yenu Maafisa Habari imetukuka, imeifanya Tanzania kupata sifa kubwa, dunia inaendelea kupata habari za Tanzania, kuijua miradi yake hasa utekelezaji wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM)" ameongeza Mhe. Abdulla

Sanjari na hayo, Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla, amewataka walengwa wa Kikao Kazi hicho ambao ni Maafisa Habari wa Serikali nchi nzima, kuzitumia mada mafunzo zitakazowasilishwa ili kufanya kazi kwa utaalam na si kufanya kazi kwa mazoea.

..............Mwisho..........






Share:

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Labels

Recent Posts

Unordered List

  • Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  • Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  • Vestibulum auctor dapibus neque.

Pages

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.