
INEC yaitaka jamii kuhamasisha amani na ushiriki katika uchaguzi Mkuu

DKT.BITEKO:TUNAWEZA KUZUIA ASILIMIA 80 YA VIFO NCHINI TUKIBADILI MTINDO WA MAISHA

RAIS SAMIA ATOA BILIONI NNE UJENZI KIWANDA CHA KUZALISHA NISHATI MBADALA

INEC YAHIMIZA viongozi wa siasa kufanya kampeni za kistaarabu

INEC yazindua rasmi kalenda ya kampeni za uchaguzi Mkuu

Kumbukumbu ya Siku ya Mashujaa Brigedia Jenerali Mstaafu Balozi Mndolwa atoa wito kwa Waandishi wa Habari kuwa Wazalendo

Ivo Mapunda kuwa Kocha Mkuu wa timu ya Taifa ‘Tembo Warriors’.

WAZIRI MKUU AMALIZA ZIARA BELARUS, ANADI FURSA ZA UWEKEZAJI NCHINI

*DKT. TULIA AFUNGUA KIKAO CHA JUKWAA LA KIBUNGE UN*

Watendaji wa uchaguzi watakiwa kutoa taarifa mapema

Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi imewataka watendaji wa uchaguzi mkuu wa mwaka 2025 kutoa taarifa mapema kwa vyama vya siasa kuhusu utaratibu wa kuwaapisha mawakala.
Tume imeyagawa mafunzo hayo kwenye awamu mbili ambapo awamu hii ya pili inahusisha mikoa ya Simiyu, Shinyanga, Kusini Pemba, Kaskazini Pemba, Mwanza, Mara, Dar es Salaam, Pwani, Rukwa, Katavi, Manyara, Arusha, Songwe na Mbeya.
Hakuna mgombea aliyekatwa,CPA Makalla awatoa hofu wagombea CCM

TBN yaipongeza Serikali kwa mafunzo maalum kwa Mabloga kuelekea uchaguzi Mkuu

Serikali kutoa mafunzo kwa waandishi wa blogu

Ns Mwandishi wetu
SERIKALI imekubali kutoa mafunzo maalum kwa waandishi wa blogu kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2025, hatua muhimu itakayowajengea uwezo na kuwaandaa kubeba dhamana kubwa ya usambazaji wa hbari sahihi.
Kauli hiyo imetolewa na Katibu Mkuu wizara ya Habari,Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa katika Mkutamo wa Wadau Kujadili Mchango wa Sekta ya habari Katika kufanikisha uchaguzi Mkuu 2025.
Katika mkutano huo kipindi cha majadiliano Mwenyekiti wa Chama cha Mabloga Tanzania (TBN), Beda Msimbe, aliomba serikali kuona umuhimu wa kufunza mabloga wengi ambao sio waandishi lakini wanatengeneza maudhui kuwa na weledi kuandika masuala ya siasa kuelekea uchaguzi mkuu.
Akizungumza kwenye mkutano huo uliofanyika Mlimani City jijini Dar es Salaam, Julai 9, 2025, Bwana Msimbe alisisitiza umuhimu wa kuwajengea uwezo mabloga, akibainisha kuwa, "Wao wanabeba dhamana kubwa kutokana na wingi wao na wanatengeneza maudhui, na wengine si waandishi wa habari."
Aliongeza kuwa katika ulimwengu wa sasa wa teknolojia na akili bandia (AI), vyanzo vya habari vinavyotegemewa zaidi si mitandao ya kijamii, bali maandishi yanayopatikana kwenye blogu na tovuti, hivyo kufanya uhitaji wa mafunzo kuwa mkubwa zaidi.
Bwana Msimbe alitumia fursa hiyo kupongeza uamuzi wa kuandaa kikao hicho muhimu cha wadau, akisema kuwa ni hatua inayostahili kuelekea uchaguzi wa haki na uwazi. Licha ya changamoto ya mada nyingi (tisa) kujadiliwa ndani ya siku moja, alipongeza mkutano huo na jinsi ulivyokwenda.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Ndugu Msigwa, aliiagiza Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuandaa mafunzo hayo mapema iwezekanavyo.
Kauli hiyo ya serikali imetafsiriwa na wadau mbalimbali kama hatua ya kutambuliwa rasmi kwa mchango wa mabloga katika tasnia ya habari na katika mchakato wa kidemokrasia.
Chama cha Mabloga Tanzania (TBN) kina wanachama zaidi ya 200 waliotawanyika kote nchini na nchi za nje, hivyo mafunzo haya yatakuwa na athari kubwa katika kuhakikisha usambazaji wa habari sahihi, zenye vigezo vya kitaaluma, na zinazozingatia maadili ya uandishi wa habari wakati wa kipindi cha uchaguzi na baadae.
Mkutano huo ulifunguliwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dk Doto Biteko ambaye alitaka vyombo vya habari na vya usalama kuhakikisha Amani na kuvumiliana kuelekea katika uchaguzi huo.
SERIKALI YAJA NA MKAKATI WA KUWAWEZESHA WAZALISHAJI CHUMVI NCHINI

MAENDELEO YA TRILIONI 5.6 YABADILI SURA YA MWANZA

Serikali yazindua mafunzo ya afya moja (ECHO)

DCEA:Hali ya dawa za kulevya nchini yazidi kuimarika,wanaotangaza ,kuhamasisha dawa za kulevya kukiona

Mfumo Mpya wa Kudhibiti Umeme Nyumbani Watengenezwa na Wanafunzi wa NIT

Na Joyce Kasiki,Dar es Salaam
WANAFUNZI wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) wameibuka na ubunifu wa kipekee kwa kutengeneza mfumo wa kisasa wa kudhibiti matumizi ya umeme majumbani, unaotumia teknolojia ya mawasiliano bila waya.
Mfumo huo, uliopewa jina la Smart Home ulioneshwa kwa mara ya kwanza kwenye Maonyesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa yanayoendelea jijini Dar es Salaam.
Akizungumza wakati wa maonyesho hayo, Sayuni Haule, mwalimu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT), alisema kuwa mfumo huo umetengenezwa na wanafunzi wake kama sehemu ya mazoezi ya vitendo yanayolenga kutafsiri elimu ya darasani kwenda kwenye maisha halisi.
Alisema kuwa mfumo huo ni mfano wa awali (prototype) unaoonesha jinsi teknolojia rahisi inaweza kutatua changamoto za kila siku za matumizi ya nishati majumbani.
“Kwa kutumia mfumo huu, mtu anaweza kuwasha au kuzima taa, feni na vifaa vingine vya umeme akiwa mbali na nyumbani kwa kutumia teknolojia ya mawasiliano isiyotumia waya,” alisema Mwalimu Haule,
“Mfano, mtu anaweza kuwa kazini au safarini na akagundua kuwa alisahau kuzima taa kwa kutumia mfumo huu, anaweza kuzima taa hizo kwa kutuma ujumbe mfupi wa maandishi (SMS) bila ya kurudi nyumbani.”
Mwalimu Haule aliongeza kuwa mfumo huu unaleta urahisi kwa watumiaji kwa kuwa unamwezesha mtu kuwa na udhibiti wa vifaa vya umeme popote alipo lakini pia ni msaada mkubwa kwa watu wenye ulemavu wa viungo kwani huwapa uwezo wa kuendesha mifumo ya nyumbani bila kulazimika kwenda moja kwa moja kwenye swichi.
Mbali na kuongeza urahisi, amesema mfumo huu pia unasaidia kudhibiti matumizi ya umeme na kupunguza gharama. “Kwa mfano, unaweza ‘kufunga’ (lock) mfumo fulani wa umeme ambao hautaki utumike kwa muda husika,umeme utakuwepo lakini hautatumika hadi ufungue tena mfumo huo,” aliongeza.
Mradi huu unaonesha uwezo mkubwa wa wanafunzi wa NIT katika kuoanisha elimu na mahitaji halisi ya jamii. ni ishara njema kwa mustakabali wa teknolojia ya ndani ya nchi na inatoa matumaini ya maendeleo ya kiteknolojia yanayoendana na mazingira ya Kitanzania
FCC yatoa elimu ya ushindani wa kibiashara, Yazindua 'Clinic' ya Biashara kwa ushauri wa faragha

REA yawataka watanzania kuachana na dhana potofu kuhusu gharama za nishati safi ya kupikia




Na Joyce Kasiki,DAR ES SALAAM
*SADC: SEKTA YA NISHATI IWE KICHOCHEO CHA KUIUNGANISHA AFRIKA KUJENGA UCHUMI*

Waziri Ridhiwani Atoa Wito kwa Vijana Kuchangamkia Fursa Zilizopo

PSPTB yatangaza Usajili wa Mitihani ya 31,wadau waombwa kujisajili mapema



Picha zote zinaonesha wajumne wa Bodi ya PSPTB wakiwa katika picha ya pamoja kwenye maonyesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara kwenye banda la PSPTB







