FCC yatoa elimu ya ushindani wa kibiashara, Yazindua 'Clinic' ya Biashara kwa ushauri wa faragha



Published from Blogger Prime Android App


Na Joyce Kasiki,DAR ES SALAAM

MAMLAKA  ya Udhibiti wa Ushindani wa Kibiashara (FCC) imetumia fursa ya maonesho ya biashara kufikisha elimu kwa wadau wa sekta ya biashara huku ikizindua 'clinic' maalum ya kutoa ushauri wa faragha kwa wafanyabiashara kuhusu masuala ya ushindani na ulinzi wa walaji.

Akizungumza katika maonesho hayo, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa FCC, Bi. Hadija Ngasongwa, alisema kuwa jukwaa hilo limewawezesha kufikia zaidi ya washiriki 3,500 kutoka sekta mbalimbali kwa lengo la kuhamasisha ushindani wenye tija na kuboresha mazingira ya uwekezaji nchini.

“FCC imeanzisha clinic ya biashara ili kutoa nafasi kwa wafanyabiashara hasa wadogo na wa kati  kupata maarifa sahihi kuhusu sheria za ushindani na haki za walaji, kwa faragha na usiri unaohitajika,” alisema Bi. Ngasongwa.

Aliongeza kuwa pamoja na kuelimisha umma, FCC inaendelea kufuatilia mwenendo wa soko na kudhibiti bidhaa bandia ambazo si tu zinahatarisha afya za walaji, bali pia zinaharibu ushindani halali katika biashara.

Ngasongwa alieleza kuwa Serikali kupitia FCC imejenga mazingira rafiki ya kufanyia biashara, hali ambayo inaendelea kuwavutia wawekezaji kutoka ndani na nje ya nchi.

 “Sheria zetu ni rafiki kwa wawekezaji, na tunajivunia kwamba Serikali imeimarisha zaidi mazingira ya biashara, jambo linalochochea ukuaji wa uchumi na uwekezaji,” alisisitiza

Alifafanua kuwa FCC inaendelea kufanya tafiti za soko zenye lengo la kuhakikisha uwiano wa ushindani unazingatiwa, pamoja na kusaidia biashara ndogo kukua hadi kufikia viwango vya juu vya ushindani.

“Dhamira yetu ni kuhakikisha kuwa siyo tu wawekezaji wa nje wanafaidika na mazingira mazuri ya biashara, bali pia wajasiriamali wa ndani wanapata nafasi ya kukuza mitaji yao kupitia ushindani wa haki,” alieleza

Maonesho hayo yamekuwa jukwaa muhimu la kubadilishana uzoefu kati ya wadau wa biashara na taasisi mbalimbali, huku FCC ikichukua hatua za makusudi kuwa karibu zaidi na wafanyabiashara kwa njia ya ushauri wa moja kwa moja na elimu ya kisheria.

Share:

No comments:

Post a Comment

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.

Labels

Blog Archive

Recent Posts

Unordered List

  • Lorem ipsum dolor sit amet, consectetuer adipiscing elit.
  • Aliquam tincidunt mauris eu risus.
  • Vestibulum auctor dapibus neque.

Pages

Theme Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.