




Picha mbalimbali zikionesha wananchi walivyotembelea na kuvutia na banda la Maliasili na utalii
Katika Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa kwa mwaka 2025 yanayofanyika katika Viwanja vya Mwalimu Julius K. Nyerere, vilivyopo barabara ya Kilwa, Jijini Dar es Salaam smbapo,kupitia maonesho haya, TAWA inatumia fursa hii kutangaza bidhaa na huduma mbalimbali zinazohusiana na utalii na uhifadhi zinazotolewa na Mamlaka hiyo.
📍Unapotembelea banda la Wizara ya Maliasili na Utalii, utakutana na maofisa wa TAWA ambao watakupa maelezo kuhusu mambo mbalimbali ikiwemo,fursa za Uwekezaji zinazopatikana katika maeneo mbalimbali yaliyo chini ya usimamizi wa TAWA, ikiwa ni pamoja na:Makuyuni Wildlife Park (Arusha),Pande (Dar es Salaam),Wami-Mbiki (Morogoro na Pwani),Tabora Zoo (Tabora),Ruhila Zoo (Ruvuma) .
Pia unapata fursa ya Kujionea Wanyamapori Hai kupitia bustani ya wanyamapori iliyopo ndani ya banda la Wizara ya Maliasili na Utalii, kwa viingilio vya bei nafuu kwa Watanzania,vivutio vya Utalii vilivyopo katika maeneo mbalimbali yanayosimamiwa na TAWA, pamoja na taarifa za gharama na namna ya kuyatembelea na ofa Maalum ya Ziara ya kutembelea Hifadhi ya Pande, iliyopo Jijini Dar es Salaam, kwa gharama nafuu katika msimu huu wa Maonesho ya Sabasaba.
Aidha ,utsona shughuli za Utalii na Uhifadhi zinazofanywa na TAWA, ikiwa ni pamoja na elimu kwa umma kuhusu namna ya kukabiliana na wanyamapori wakali na waharibifu, na kuelewa tabia zao na fursa ya Kufurahia Nyamapori Choma iliyoandaliwa kwa umahiri na kwa kuzingatia ubora wa hali ya juu Kwa bei ya kizalendo.
Wananchi wote mnakaribishwa kkwa wingi katika banda la Wizara ya Maliasili na Utalii, mjifunze, muelimike na mjionee huduma na vivutio vya kipekee, hasa wanyamapori hai waliopo ndani ya banda hilo.
No comments:
Post a Comment